-
Masomo Yenye Kutumika Kutokana na Bara LililoahidiwaMnara wa Mlinzi—1996 | Agosti 15
-
-
Vilima vya Karmeli
Jina Karmeli humaanisha “Shamba la Matunda.” Eneo hili lenye rutuba, kuelekea magharibi, urefu wa karibu kilometa 50 hivi, limerembwa kwa mashamba ya mizabibu, miti ya mizeituni, na miti ya matunda. Safu hiyo yenye vilima-vilima hukumbukwa kwa sababu ya uzuri na urembo wayo. Isaya 35:2 husema juu ya “uzuri wa Karmeli” ikiwa ishara ya utukufu wenye kuzaa wa bara lililorudishwa la Israeli.
-
-
Masomo Yenye Kutumika Kutokana na Bara LililoahidiwaMnara wa Mlinzi—1996 | Agosti 15
-
-
Mitelemko ya Karmeli bado ina mashamba ya matunda, miti ya mizeituni, na mizabibu. Wakati wa vuli, mitelemko hii hufunikwa na wonyesho mzuri sana wa maua. “Kichwa chako juu yako ni kama Karmeli,” Sulemani akamwambia mwanamwali Mshulami, alipokuwa anarejezea uzuri wa nywele zake au kichwa chake kizuri kilichotokeza kwa fahari kutoka kwenye shingo yake.—Wimbo Ulio Bora 7:5.
Uzuri ambao ulionyeshwa na vilima vya Karmeli hutukumbusha juu ya uzuri wa kiroho ambao Yehova amelitolea tengenezo la waabudu wake wa kisasa. (Isaya 35:1, 2) Kwa kweli Mashahidi wa Yehova huishi katika paradiso ya kiroho, wao hukubaliana na maneno ya hisia ya Mfalme Daudi, ambaye aliandika: “Kamba zangu zimeniangukia mahali pema, Naam, nimepata urithi mzuri.”—Zaburi 16:6.
-