-
Tuna Sababu ya Kulia kwa ShangweMnara wa Mlinzi—1996 | Februari 15
-
-
“Wao watapata mchachawo na kushangilia, na huzuni na kupiga kite lazima zikimbie mbali.”—ISAYA 35:10, NW.
-
-
Tuna Sababu ya Kulia kwa ShangweMnara wa Mlinzi—1996 | Februari 15
-
-
3. Ni maneno gani yenye maana yanayostahili uangalifu wetu, na kwa nini?
3 Kumbuka maneno haya ya Yesu: “Mambo hayo nimewaambia, ili shangwe yangu ipate kuwa katika nyinyi na shangwe yenu ipate kufanywa yenye kujaa.” (Yohana 15:11, NW) “Shangwe yenu ipate kufanywa yenye kujaa.” Huo ni ufafanuzi ulioje! Funzo la kindani juu ya njia ya kuishi ya Kikristo lingefunua sababu nyingi za kujaa kwa shangwe yetu. Lakini sasa hivi, ona maneno yenye maana kwenye Isaya 35:10 (NW). Haya ni yenye maana kwa sababu yanahusiana sana nasi leo. Twasoma hivi: “Wale wenyewe waliokombolewa na Yehova watarudi na kwa hakika watakuja Zayoni kwa kilio chenye shangwe; na kushangilia hadi wakati usio dhahiri kutakuwa juu ya kichwa chao. Wao watapata mchachawo na kushangilia, na huzuni na kupiga kite lazima zikimbie mbali.”
4. Ni shangwe ya namna gani inayotajwa kwenye Isaya 35:10, na kwa nini tukazie jambo hilo uangalifu?
4 “Kushangilia hadi wakati usio dhahiri.” Fungu la maneno “hadi wakati usio dhahiri” ni ufasiri sahihi wa kile ambacho Isaya aliandika katika Kiebrania. Lakini, kama vile imeonyeshwa katika maandiko mengine, maana yalo katika mstari huu ni “milele.” (Zaburi 45:6; 90:2; Isaya 40:28) Kwa hiyo kushangilia huko kutakuwa bila kikomo, katika hali zitakazoruhusu—ndiyo, zitakazothibitisha—kushangilia kudumuko milele. Je, hilo halisikiki kuwa jambo lenye kupendeza? Lakini, labda mstari huo waonekana kwako kuwa simulizi juu ya hali ya kuwaziwa tu, likikufanya uhisi: ‘Hilo kwa kweli halinihusu mimi kadiri ambavyo matatizo na mahangaiko yangu ya kila siku hunihusu.’ Lakini, mambo ya hakika huonyesha vingine. Ahadi ya kiunabii kwenye Isaya 35:10 ina maana kwako leo. Ili kupata kujua ni jinsi gani, acheni tuchunguze sura hii nzuri, Isaya 35, tukiangalia kila sehemu kulingana na muktadha. Uwe na uhakika kwamba utafurahia kile tutakachopata.
-