-
Wenye Kufariji UnaokuhusuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
6. Nabii anamfafanuaje mshindi wa wakati ujao?
6 Kupitia Isaya, Yehova anatabiri mshindi atakayeokoa watu wa Mungu kutoka Babiloni na pia ahukumu adui zao. Yehova anauliza hivi : “Ni nani aliyemwinua mmoja atokaye mashariki, ambaye katika haki amemwita mguuni pake? ampa mataifa mbele yake, na kumtawaza juu ya wafalme [“kumfanya aende akitiisha hata wafalme,” “NW”]; awatoa wawe kama mavumbi kwa upanga wake, kama makapi yaliyopeperushwa kwa upinde wake. Awafuatia, apita salama hata kwa njia asiyoikanyaga kamwe kwa miguu yake. Ni nani aliyetenda na kufanya jambo hilo, aviitaye vizazi tangu mwanzo? Mimi, BWANA, wa kwanza na wa mwisho, mimi ndiye.”—Isaya 41:2-4.
-
-
Wenye Kufariji UnaokuhusuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
8. Ni Yehova tu anayeweza kufanya nini?
8 Hivyo, Yehova anamtumia Isaya kutabiri kuinuka kwa Koreshi, zamani kabla mfalme huyo hajazaliwa. Ni Mungu wa kweli tu anayeweza kutoa unabii kama huo kwa usahihi. Hakuna aliye sawa na Yehova kati ya miungu ya uwongo ya mataifa. Basi Yehova ana sababu nzuri ya kusema hivi: “Utukufu wangu sitampa mwingine.” Yehova tu ndiye mwenye haki ya kusema hivi: “Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho; zaidi yangu mimi hapana Mungu.”—Isaya 42:8; 44:6, 7.
-