Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 6. Jinsi Yehova anavyowasaidia rafiki zake

      Yehova huwasaidia rafiki zake kukabiliana na matatizo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Yehova Amenisaidia Sana (3:21)

      • Yehova amemsaidiaje mwanamke katika video hiyo kukabiliana na mawazo na hisia zisizofaa?

      Soma Isaya 41:10, 13, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Yehova anaahidi kuwafanyia nini rafiki zake wote?

      • Je, unafikiri Yehova ni rafiki mzuri? Kwa nini?

      Picha: Marafiki wa karibu wakisaidiana. 1. Wanaume wakisaidiana kubeba meza. 2. Mwanamke akimweleza mwanamke mwenzake mahangaiko yake. 3. Mwanamume akimsaidia mwenzake aliyevunjika mguu kutembea.

      Rafiki wa karibu watakusaidia unapohitaji msaada. Yehova pia atakusaidia

  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Yehova
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Unawezaje Kuwahubiria Wengine Habari Njema?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 3. Yehova atakuwa pamoja nawe

      Huenda baadhi ya wanafunzi wa Biblia wanaotaka kuanza kuhubiri, wakahangaishwa na jinsi watu watakavyowaona, au jinsi watu watakavyoitikia ujumbe.

      • Je, wewe unaogopa kuwaambia wengine mambo unayojifunza? Kwa nini?

      Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Nilimwomba Yehova Anipe Ujasiri (4:05)

      • Vijana hao Mashahidi walishindaje woga wao?

      Soma Isaya 41:10, kisha mzungumzie swali hili:

      • Sala inaweza kukusaidiaje ikiwa unaogopa kuhubiri?

      Je, wajua?

      Kabla ya kuanza kuhubiri habari njema, Mashahidi wengi wa Yehova walifikiri hawawezi kamwe kufanya kazi hiyo. Kwa mfano, Sergey alihisi kwamba hafai na ilikuwa vigumu kwake kuzungumza na watu. Lakini baada ya kujifunza Biblia alisema hivi: “Ingawa nilikuwa na woga, nilianza kuwaeleza wengine kuhusu mambo niliyokuwa nikijifunza. Kwa kushangaza, nilipozungumza na wengine kuhusu Biblia nilipata ujasiri zaidi. Pia, imani yangu iliimarika hata zaidi.”

  • Je, Uko Tayari Kubatizwa?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 6. Uwe na hakika kwamba Yehova atakusaidia

      Mwanamke huyo akimhubiria mwanamke aliyezeeka. Mwalimu wake wa Biblia ameambatana naye katika huduma.

      Yehova atakusaidia kufanya mambo yanayomfurahisha. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Yehova Mungu Atakusaidia (2:50)

      • Katika video hiyo, ni nini kilichofanya mwanafunzi huyo wa Biblia asite kubatizwa?

      • Alijifunza jambo gani ambalo lilimsaidia kumtegemea Yehova zaidi?

      Soma Isaya 41:10, 13, kisha mzungumzie swali hili:

      • Unawezaje kuwa na hakika kwamba utatimiza ahadi unayotoa unapojiweka wakfu?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki