-
Tazama! Mtumishi wa Yehova AliyekubaliwaMnara wa Mlinzi—2009 | Januari 15
-
-
4 Yesu alipokuwa mtoto, mwanamume fulani mwadilifu aliyeitwa Simeoni alitangaza huku akiongozwa na roho takatifu kwamba “mtoto mchanga Yesu” atakuwa “nuru ya kuondoa utaji kwa mataifa,” kama ilivyotabiriwa katika Isaya 42:6 na 49:6. (Luka 2:25-32) Zaidi ya hayo, unabii ulio katika Isaya 50:6-9 ulitabiri mateso yenye kufedhehesha yaliyompata Yesu usiku ambao kesi yake ilifanywa. (Mt. 26:67; Luka 22:63) Baada ya Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K., mtume Petro alimtambulisha Yesu waziwazi kuwa “Mtumishi” wa Yehova. (Isa. 52:13; 53:11; soma Matendo 3:13, 26.) Tunaweza kujifunza nini katika unabii huo mbalimbali kumhusu Masihi?
-
-
Tazama! Mtumishi wa Yehova AliyekubaliwaMnara wa Mlinzi—2009 | Januari 15
-
-
“Nuru” na “Agano”
11. Ni kwa njia gani Yesu alikuwa “nuru ya mataifa” katika karne ya kwanza, na leo pia?
11 Kwa kweli, Yesu alikuwa “nuru ya mataifa,” na hivyo akatimiza unabii wa Isaya 42:6. Wakati wa huduma yake duniani, alileta nuru ya kiroho hasa kwa Wayahudi. (Mt. 15:24; Mdo. 3:26) Lakini Yesu alisema hivi: “Mimi ndiye nuru ya ulimwengu.” (Yoh. 8:12) Alikuwa nuru kwa Wayahudi na kwa mataifa si tu kwa kuwapa nuru ya kiroho bali pia kwa kudhabihu uhai wake mkamilifu akiwa mwanadamu ili awe dhabihu ya ukombozi kwa ajili ya wanadamu wote. (Mt. 20:28) Baada ya ufufuo wake, aliwaagiza wanafunzi wake wawe mashahidi wake “mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Wakati wa huduma yao, Paulo na Barnaba walitaja maneno “nuru ya mataifa” na kuutumia kuhusu kazi ya kuhubiri ambayo walikuwa wakifanya kati ya watu wasio Wayahudi. (Mdo. 13:46-48; linganisha na Isaya 49:6.) Kazi hiyo bado inafanywa na ndugu za Yesu watiwa-mafuta walio duniani na waandamani wao ambao wanasambaza nuru ya kiroho na kuwasaidia watu kumwamini Yesu, ambaye ndiye “nuru ya mataifa.”
12. Yehova amemtoa jinsi gani Mtumishi wake “kuwa agano la watu”?
12 Katika unabii huohuo, Yehova alimwambia hivi Mtumishi wake mchaguliwa: “Nitakulinda na kukutoa kuwa agano la watu.” (Isa. 42:6) Shetani alijitahidi sana kumwangamiza Yesu na kumzuia asimalize huduma yake duniani, lakini Yehova alimlinda mpaka wakati uliowekwa wa kifo chake. (Mt. 2:13; Yoh. 7:30) Kisha Yehova akamfufua Yesu na kumtoa kuwa “agano,” au ahadi, kwa watu walio duniani. Ahadi hiyo rasmi ilitoa uhakikisho wa kwamba Mtumishi huyo mwaminifu wa Mungu angeendelea kuwa “nuru ya mataifa,” na hivyo kuwaweka huru wale walio katika giza la kiroho.—Soma Isaya 49:8, 9.b
-