Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wachukuaji Nuru—Kwa Kusudi Gani?
    Mnara wa Mlinzi—1993 | Januari 15
    • Yule Aliyetolewa Kuwa “Nuru ya Mataifa”

      6. Yehova ametuwezesha tuwe na matarajio gani matukufu kupitia Yesu Kristo?

      6 Hata kabla ya Adamu na Hawa kuondolewa katika Paradiso, Yehova alitabiri kuhusu “mbegu” ambayo ingekuwa mkombozi wa wapendao uadilifu. (Mwanzo 3:15, NW) Kufuatia kuzaliwa kwa kibinadamu kwa hiyo Mbegu iliyoahidiwa, Yehova alimfanya Simeoni mzee, kwenye hekalu katika Yerusalemu, amtambulishe huyo kuwa ndiyo “nuru ya kuwa mwangaza [ya kuondolea shela, NW] kwa Mataifa.” (Luka 2:29-32) Kupitia imani katika dhabihu ya Yesu ya uhai mkamilifu wa kibinadamu, wanadamu wangeweza kuondolewa laana iliyotokana na dhambi ya kuzaliwa. (Yohana 3:36) Kupatana na mapenzi ya Yehova, wangeweza kutazamia uhai wa milele katika ukamilifu wakiwa sehemu ya Ufalme wa kimbingu au wakiwa raia za Ufalme huo katika dunia paradiso. Huo ni uandalizi mzuri ajabu jinsi gani!

      7. Kwa nini ahadi kwenye Isaya 42:1-4 pamoja na utimizo wayo wa karne ya kwanza unatujaza tumaini?

      7 Yesu Kristo mwenyewe ndiye dhamana ya kutimizwa kwa mataraja hayo matukufu. Kuhusiana na kuponya kwa Yesu watu waliosumbuliwa, mtume Mathayo alitumia yale yaliyoandikwa kwenye Isaya 42:1-4 kumhusu yeye. Andiko hilo lasema hivi kwa sehemu: “Tazama mtumishi wangu nimtegemezaye; mteule wangu, ambaye nafsi yangu imependezwa naye; nimetia roho yangu juu yake; naye atawatolea mataifa hukumu.” Na je! hilo silo jambo ambalo watu wa mataifa yote wanahitaji? Unabii huo waendelea hivi: “Hatalia, wala hatapaza sauti yake, wala kuifanya isikiwe katika njia kuu. Mwanzi uliopondeka hatauvunja, wala utambi utokao moshi hatauzima.” Kupatana na hilo, Yesu hakutenda kikatili watu waliokuwa tayari wamesumbuka. Aliwaonyesha huruma, akawafundisha makusudi ya Yehova, na kuwaponya magonjwa yao.—Mathayo 12:15-21.

      8. Yesu ametolewa katika maana gani na Yehova awe “agano la watu” na “nuru ya mataifa”?

      8 Mpaji wa unabii huo anaelekeza fikira zake kwa Mtumishi wake, Yesu, na kusema: “Mimi, BWANA [Yehova, NW], nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa; kuyafunua macho ya vipofu, kuwatoa gerezani waliofungwa, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufungwa.” (Isaya 42:6, 7) Naam, Yehova ametoa Yesu Kristo awe agano, awe dhamana nzito ya kiahadi. Jinsi hilo linavyotia moyo! Yesu alionyesha hangaikio la kweli kwa ainakibinadamu alipokuwa duniani; hata alitoa uhai wake kwa ajili ya ainabinadamu. Huyo ndiye yule ambaye Yehova amekabidhi utawala juu ya mataifa yote. Si ajabu kwamba Yehova alisema juu yake kuwa nuru ya mataifa. Yesu mwenyewe alisema: “Mimi ndimi nuru ya ulimwengu.”—Yohana 8:12.

      9. Kwa nini Yesu hakujitoa mwenyewe kufanyia maendeleo mfumo wa mambo wa wakati huo?

      9 Yesu alitumika akiwa “nuru ya ulimwengu” kwa kusudi gani? Kwa kweli haikuwa kwa kusudi lolote la kilimwengu au la kutaka vitu vya kimwili. Yeye alikataa kujaribu kunyorosha mfumo wa kisiasa wa wakati huo kwa kutokubali ufalme ama kutoka kwa Shetani, mtawala wa ulimwengu, ama kutoka kwa watu. (Luka 4:5-8; Yohana 6:15; 14:30) Yesu alionyesha huruma nyingi kwa wale waliokuwa na masumbufu, akawapa kitulizo kwa njia ambazo wengine wasingeweza. Lakini alijua kwamba kitulizo cha kudumu hakingewezekana katika muundo wa jamii ya kibinadamu iliyokuwa chini ya laana ya kimungu kwa sababu ya dhambi ya kuzaliwa na iliyokuwa chini ya uvutano wa nguvu zisizoonekana za roho waovu. Akiwa na mwono-ndani wa kimungu, Yesu alitumia maisha yake hasa katika kufanya mapenzi ya Mungu.—Waebrania 10:7.

      10. Yesu alitumika akiwa nuru ya ulimwengu katika njia zipi na kwa kusudi gani?

      10 Basi, Yesu alitumika akiwa nuru ya ulimwengu katika njia zipi na kwa kusudi gani? Yeye alijitoa mwenyewe kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. (Luka 4:43; Yohana 18:37) Kwa kutoa ushahidi kuhusu kweli ya kusudi la Yehova, Yesu pia alitukuza jina la Baba yake wa kimbingu. (Yohana 17:4, 6) Isitoshe, akiwa nuru ya ulimwengu, Yesu alifunua uwongo wa kidini na hivyo akaandaa uhuru wa kiroho kwa wale waliokuwa katika ufungwa wa kidini. Alimfunua Shetani kuwa yule asiyeonekana mwenye uvutano juu ya wale wanaojiruhusu watumiwe naye. Yesu pia alitambulisha wazi matendo ya giza. (Mathayo 15:3-9; Yohana 3:19-21; 8:44) Kwa kutokeza, yeye alithibitika kuwa nuru ya ulimwengu kwa kutoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu kuwa fidia, kwa namna hiyo akifungulia njia wale wanaojizoeza imani katika uandalizi huo wapate msamaha wa dhambi, uhusiano wenye kibali cha Mungu, na taraja la uhai wa milele wakiwa sehemu ya familia ya Yehova ya ulimwengu wote mzima. (Mathayo 20:28; Yohana 3:16) Na hatimaye, kwa kudumisha ujitoaji kimungu ulio mkamilifu katika maisha yake yote, Yesu alitegemeza enzi kuu ya Yehova na kumthibitisha Ibilisi kuwa mwongo, kwa njia hiyo akiwezesha wapendao uadilifu kupata faida za milele. Lakini, je! Yesu angekuwa ndiye mchukuaji nuru pekee?

  • Wachukuaji Nuru—Kwa Kusudi Gani?
    Mnara wa Mlinzi—1993 | Januari 15
    • 12. (a) Nuru ya kiroho ilitazamiwa ienee mbali kadiri gani? (b) Roho ya Yehova ilimwezesha Paulo atambue nini kuhusu Isaya 42:6, na unabii huo unapaswa uathirije maisha zetu?

      12 Hata hivyo, kuhubiriwa kwa habari hizo njema hakungefanywa kwenye shamba hilo pekee. Yesu aliagiza wafuasi wake ‘wawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi.’ (Mathayo 28:19) Wakati wa kugeuzwa kwa Saulo wa Taso, Bwana alionyesha kihususa kwamba Saulo (ambaye baadaye akawa mtume Paulo) angehubiri si kwa Wayahudi peke yao bali pia kwa wasio Wayahudi. (Matendo 9:15) Kwa msaada wa roho takatifu, Paulo alikuja kufahamu yale yaliyohusishwa na hilo. Hivyo, akafahamu kwamba unabii kwenye Isaya 42:6, unaotimizwa moja kwa moja katika Yesu Kristo, pia ni amri iliyokusudiwa wote wanaojizoeza imani katika Kristo. Kwa hiyo, kwenye Matendo 13:47, alipomnukuu Isaya, Paulo alisema hivi: “Ndivyo tulivyoamriwa na Bwana [Yehova, NW], Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.” Namna gani wewe? Je! umefikiria kibinafsi kwa uzito wajibu huo wa kuwa mchukuaji nuru? Kama vile Yesu na mtume Paulo, je, wewe hutumia maisha yako kufanya mapenzi ya Mungu?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki