Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 7 Naam, Yehova ndiye mmilikaji wa shamba hilo la mizabibu, naye ni kama mtu anayeenda mahakamani, akitaka hukumu itolewe kati yake na shamba lake la mizabibu linalokatisha tamaa. Basi, shamba hilo la mizabibu ni nini? Mmilikaji aeleza: “Shamba la mizabibu la BWANA wa majeshi ndilo nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni mche wake wa kupendeza.”—Isaya 5:7a.

  • Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Kutambua Shamba la Mizabibu la Mungu Leo

      10. Yesu alitoa mfano gani unaohusu shamba la mizabibu?

      10 Huenda Yesu alikuwa akizingatia maneno ya Isaya alipotoa mfano wa walimaji wauaji: “Kulikuwa na mtu, mwenye nyumba, aliyepanda shamba la mizabibu na kuweka ua kulizunguka naye akachimba sindikio la divai katika hilo akasimamisha mnara, na kulikodisha kwa walimaji, na kusafiri nchi ya nje.” Kwa kuhuzunisha, walimaji hao walimsaliti mmilikaji wa shamba hilo la mizabibu, hata wakamwua mwanaye. Kisha Yesu akaonyesha kuwa mfano huo ulihusisha mengi kuliko tu Israeli halisi, aliposema hivi: “Ufalme wa Mungu utachukuliwa kutoka kwenu [Israeli la kimwili] na kupewa kwa taifa lenye kutokeza matunda yao.”—Mathayo 21:33-41, 43.

      11. Ni shamba gani la mizabibu la kiroho lililokuwapo katika karne ya kwanza, lakini ni nini kilichotukia baada ya kifo cha mitume?

      11 “Taifa” jipya hilo lilithibitika kuwa “Israeli wa Mungu”—taifa la kiroho la Wakristo watiwa-mafuta lenye idadi ya jumla ya 144,000. (Wagalatia 6:16; 1 Petro 2:9, 10; Ufunuo 7:3, 4) Yesu aliwafananisha wanafunzi hao na “matawi” katika “mzabibu wa kweli,” yaani, yeye mwenyewe. Kwa kawaida, matawi hayo hutarajiwa kuzaa matunda. (Yohana 15:1-5) Ni lazima wadhihirishe sifa kama za Kristo na kuishiriki kazi ya kuhubiri “habari njema hii ya ufalme.” (Mathayo 24:14; Wagalatia 5:22, 23) Lakini tangu kifo cha wale mitume kumi na wawili, wengi wa wale wanaodai kuwa matawi ya “mzabibu wa kweli” wamethibitika kuwa bandia—kwa kuzaa zabibu-mwitu badala ya matunda mema.—Mathayo 13:24-30, 38, 39.

      12. Maneno ya Isaya yahukumuje Jumuiya ya Wakristo, nayo yana fundisho gani kwa Wakristo wa kweli?

      12 Kwa hiyo, shutuma ya Isaya juu ya Yuda yahusu Jumuiya ya Wakristo leo. Uchunguzi wa historia yake—vita zake, krusedi zake, Mabaraza yake ya Kuhukumu Wazushi—wafunua kadiri ambayo matunda yake yamekuwa machungu! Hata hivyo, shamba la mizabibu la kweli la Wakristo watiwa-mafuta pamoja na waandamani wao wa “umati mkubwa” lazima watii maneno ya Isaya. (Ufunuo 7:9) Iwapo watampendeza mmilikaji wa shamba la mizabibu, ni lazima wao, mmoja-mmoja na pia wakiwa kikundi, wazae matunda yanayompendeza.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki