Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Ninyi Ni Mashahidi Wangu”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 11. Ni agizo gani ambalo Yehova anampa mtumishi wake, na Yehova anafunua nini juu ya Uungu wake?

      11 Miungu ya uwongo haiwezi kutokeza mashahidi maana haiwezi kitu. Basi aibu ndiyo hiyo, kizimba cha ushahidi kinabaki tupu. Lakini sasa ni wakati wa Yehova kuthibitisha Uungu wake. Akiwatazama watu wake, anasema hivi: “Ninyi ni mashahidi wangu, . . . na mtumishi niliyemchagua; mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine. Mimi, naam, mimi, ni BWANA [“Yehova,” “NW”], zaidi yangu mimi hapana mwokozi. Nimetangaza habari, nimeokoa, nimeonyesha, na hapakuwa mungu wa kigeni kati yenu; kwa sababu hiyo ninyi ni mashahidi wangu, . . . nami ni Mungu. Naam, tangu siku ya leo, mimi ndiye; wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu; mimi nitatenda kazi, naye ni nani awezaye [kuuzuia mkono wangu]?”—Isaya 43:10-13.

      12, 13. (a) Watu wa Yehova wana ushuhuda gani mwingi wa kutoa? (b) Jina la Yehova limetokeaje waziwazi nyakati za kisasa?

      12 Kwa kuyaitikia maneno ya Yehova, umati wa mashahidi wenye shangwe unajaa upesi kizimbani. Ushuhuda wao ni wazi na hauwezi kukanushwa. Wao, kama vile Yoshua, wanashuhudia kwamba ‘yote aliyonena Yehova yametimia. Hapana neno lo lote limepungua.’ (Yoshua 23:14) Bado watu wa Yehova wanayakumbuka maneno ya Isaya, Yeremia, Ezekieli, na manabii wengine waliotabiri, kana kwamba ni kwa sauti moja, kuhamishwa kwa Yuda kisha kukombolewa kwao kimwujiza. (Yeremia 25:11, 12) Koreshi, mkombozi wa Yuda, alitajwa jina mapema sana hata kabla hajazaliwa!—Isaya 44:26–45:1.

      13 Ushuhuda chungu nzima umetolewa, basi nani atakataa kwamba Yehova ndiye Mungu wa pekee wa kweli? Ni Yehova tu asiyeumbwa, tofauti na miungu ya kipagani; ni yeye tu Mungu wa kweli.a Basi, watu wanaoitwa kwa jina la Yehova wana pendeleo la kipekee, tena la kusisimua, kusimulia maajabu yake kwa vizazi vya wakati ujao, na kwa wengine wanaoulizia habari zake. (Zaburi 78:5-7) Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova wa kisasa wana pendeleo la kutangaza jina la Yehova duniani pote. Miaka ya 1920, Wanafunzi wa Biblia walizidi kufahamu umaana mkubwa wa jina la Mungu, Yehova. Kisha, Julai 26, 1931, kwenye mkusanyiko kule Columbus, Ohio, msimamizi wa Sosaiti, Joseph F. Rutherford, akatokeza azimio lenye kichwa “Jina Jipya.” Yale maneno, “Nasi twataka tujulikane na kuitwa kwa jina hili, yaani, mashahidi wa Yehova,” yalisisimua wahudhuriaji, sauti zao zikavuma “Ndiyo!” kwa kukubali azimio hilo. Tangu hapo, jina la Yehova limesifika ulimwenguni pote.—Zaburi 83:18.

  • “Ninyi Ni Mashahidi Wangu”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • a Katika hadithi za mataifa, miungu mingi “huzaliwa” na huzaa “watoto.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki