Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 25, 26. Isaya afunua hali gani mbovu ya kufikiri kwa Waisraeli katika ole wa tatu na wa nne?

      25 Sasa sikiliza ole wa tatu na wa nne wa Isaya: “Ole wao wavutao uovu kwa kamba za ubatili, na dhambi kama kwa kamba za gari! Wasema, Na afanye haraka, aihimize kazi yake, tupate kuiona; na likaribie shauri lake aliye Mtakatifu wa Israeli, tupate kuliona. Ole wao wasemao kwamba uovu ni wema, na kwamba wema ni uovu; watiao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza; watiao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu!”—Isaya 5:18-20.

      26 Hiyo yawafafanua kinaganaga kama nini wale wanaozoea dhambi! Wameshikamana na dhambi kama vile wanyama wavutao mizigo wanavyofungwa kwenye magari. Watenda-dhambi hao hawaogopi siku yoyote ya hukumu inayokuja. Wao wasema kwa dhihaka: “[Mungu] na . . . aihimize kazi yake”! Badala ya kuitii Sheria ya Mungu, wao hupotoa mambo, wakitangaza kuwa “uovu ni wema, na kwamba wema ni uovu.”—Linganisha Yeremia 6:15; 2 Petro 3:3-7.

  • Ole kwa Shamba la Mizabibu Lisilo na Uaminifu!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • [Picha katika ukurasa wa 83]

      Mtenda-dhambi ameshikamana na dhambi kama vile mnyama avutaye mizigo anavyofungwa kwenye gari

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki