-
Kumtambua Mjumbe wa Aina InayofaaMnara wa Mlinzi—1997 | Mei 1
-
-
10. Sairasi alikuwa “mtiwa-mafuta” kwa njia gani, na Yehova angeweza kusemaje naye miaka zaidi ya mia moja kabla ya kuzaliwa kwake?
10 Ona kwamba Yehova anasema na Sairasi kana kwamba tayari yuko hai. Hilo lapatana na taarifa ya Paulo kwamba Yehova “huita mambo yasiyokuwako kama kwamba yamekuwako.” (Waroma 4:17) Pia, Mungu amtambua Sairasi kuwa “mtiwa-mafuta” wake. Kwa nini alifanya hivyo? Kwa vyovyote, kuhani wa Yehova wa cheo cha juu hakutia kamwe mafuta matakatifu kwenye kichwa cha Sairasi. Ni kweli, lakini huku ni kutiwa mafuta kwa kiunabii. Huonyesha kuwekwa rasmi, kuingizwa katika cheo cha pekee. Kwa hiyo Mungu angeweza kusema juu ya tendo lake la kumweka rasmi Sairasi kimbele kuwa kama kutiwa mafuta.—Linganisha 1 Wafalme 19:15-17; 2 Wafalme 8:13.
-
-
Kumtambua Mjumbe wa Aina InayofaaMnara wa Mlinzi—1997 | Mei 1
-
-
12, 13. Maneno ya Yehova kupitia mjumbe wake Isaya yalitimiaje wakati Babiloni lilipoanguka mikononi mwa Sairasi?
12 Walakini Wayahudi walio mateka waliokuwa na imani katika Yehova hawakukata tamaa! Walikuwa na tumaini jangavu. Kupitia manabii wake, Mungu alikuwa ameahidi kuwaweka huru. Mungu alitimizaje ahadi yake? Sairasi aliamuru majeshi yake yageuzie mbali mkondo wa Mto Frati mahali fulani, kilometa nyingi kaskazini ya Babiloni. Hivyo, ulinzi mkuu wa hilo jiji ukawa sakafu ya mto iliyokauka kwa kadiri fulani. Usiku huo wa maana, walevi waliokuwa wakinywa humo Babiloni waliacha bila kujali ile milango yenye sehemu mbili kandokando ya sehemu ya jiji iliyokuwa ikikabili Frati. Yehova hakuivunja ile milango ya shaba vipande vipande kihalisi; wala hakuyakata-kata mapingo ya chuma yenye kuifunga, lakini mbinu yake ya kuiacha ikiwa wazi bila kuzuiwa ilikuwa na matokeo hayohayo. Kuta za Babiloni zilikuwa bure. Vikosi vya Sairasi havikuhitaji kuzipanda kuta hizo ili kuingia ndani. Yehova alikwenda mbele ya Sairasi, akipasawazisha “mahali palipoparuza,” ndiyo, vizuizi vyote. Isaya alithibitishwa kuwa mjumbe wa kweli wa Mungu.
-