Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova—“Mungu Mwenye Haki, Mwokozi”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 24, 25. (a) Yehova anatoa mwaliko gani, na kwa nini ni hakika kwamba ahadi yake itatimizwa? (b) Yehova anataka apewe nini kilicho haki yake?

      24 Rehema ya Yehova humsukuma kutoa mwaliko huu: “Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine. Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa. Mmoja ataniambia, Kwa BWANA, peke yake, iko haki [“kamili,” “NW”] na nguvu; naam, watu watamwendea yeye, na wote waliomkasirikia watatahayarika. Katika BWANA wazao wote wa Israeli watapewa haki, na kutukuka [“kujisifu juu yao wenyewe,” “NW”].”—Isaya 45:22-25.

  • Yehova—“Mungu Mwenye Haki, Mwokozi”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 26. “Umati mkubwa” kutoka kwenye mataifa yote unaitikiaje mwaliko wa Yehova kwamba wamgeukie?

      26 Hata hivyo, si wahamishwa walioko Babiloni peke yao wanaopewa mwaliko wa Mungu wamgeukie. (Matendo 14:14, 15; 15:19; 1 Timotheo 2:3, 4) Mwaliko huo ungali ukitolewa, na “umati mkubwa . . . kutoka katika mataifa yote” unaitikia na kutangaza hivi: ‘Sisi tunawiwa wokovu na Mungu wetu na Mwana-Kondoo,’ Yesu. (Ufunuo 7:9, 10; 15:4) Kila mwaka, mamia ya maelfu ya wapya huipanua idadi ya umati mkubwa kwa kumgeukia Mungu, wakitambua kikamili enzi yake kuu na kutangaza peupe ushikamanifu wao kwake. Zaidi ya hilo, wao huwaunga mkono Israeli wa kiroho, “mbegu ya Abrahamu.” (Wagalatia 3:29) Wao huonyesha wanaupenda utawala mwadilifu wa Yehova kwa kutangaza ulimwenguni pote hivi: ‘Kwa BWANA, peke yake, iko haki na nguvu kamili.’a Katika barua yake kwa Waroma, mtume Paulo alinukuu tafsiri ya Septuagint ya Isaya 45:23 kuonyesha kwamba hatimaye kila mtu aliye hai atakiri enzi kuu ya Mungu na kusifu jina lake kwa uendelevu.—Waroma 14:11; Wafilipi 2:9-11; Ufunuo 21:22-27.

  • Yehova—“Mungu Mwenye Haki, Mwokozi”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • a Biblia ya New World Translation hutumia usemi “uadilifu kamili” kwa sababu maandishi ya Kiebrania yanaonyesha neno “uadilifu” kwa namna ya wingi. Hapa wingi umetumiwa kuonyesha utele wa uadilifu wa Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki