Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 12. Kwa nini Babiloni anaitwa ‘mwanamke apendaye anasa’?

      12 Yehova anatangaza rasmi hivi: “Sasa, basi, sikia haya, wewe [“mwanamke,” “NW”] upendaye anasa, ukaaye na kujiona salama, wewe usemaye moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi; sitaketi mfano wa mjane, wala sitajua kufiwa na watoto.” (Isaya 47:8) Babiloni amevuma sana kwa kutafuta anasa. Mwanahistoria Herodotus wa karne ya tano K.W.K. anaelezea “desturi ya aibu sana” ya Wababiloni, ya kwamba wanawake wote walitakiwa kufanya umalaya ili kuonyesha kwamba wanamheshimu sana mungu wao wa kike wa mapenzi. Naye Curtius, mwanahistoria wa kale, alisema hivi: “Uchafu wa jiji hilo hauna kifani; hakuna zoea la ufisadi liwezalo kuwachochea watu na kuamsha tamaa zao za uasherati kwa kiwango kile.”

      13. Mwelekeo wa Babiloni wa kutafuta anasa utaharakishaje anguko lake?

      13 Mwelekeo wa Babiloni wa kutafuta anasa utaharakisha anguko lake. Muda mfupi kabla ya anguko lake, mfalme wa Babiloni na watu wenye vyeo watakula karamu, wanywe walewe chakari. Hivyo, hawatayajali hata kidogo majeshi ya Umedi-Uajemi yanayolivamia jiji. (Danieli 5:1-4) ‘Akiwa amekaa kwa kujiona salama,’ Babiloni atawaza kwamba hawezi kuvamiwa kwani kuta zake na handaki lake lenye maji zinampa himaya inayoonekana kuwa isiyopenyeka. Anajiambia kwamba “hapana mwingine” kamwe wa kutwaa cheo chake cha ukuu. Hafikiri kwamba angeweza kuwa “mjane,” afiwe na maliki wake, na vilevile “watoto” au wananchi wake. Vyovyote vile, hakuna ukuta uwezao kumhami kutokana na mkono wa Yehova Mungu wa kulipiza kisasi! Yehova atasema hivi baadaye: “Babeli ujapopanda mbinguni, na ujapopafanya mahali pa juu penye nguvu zake kuwa ngome, hata hivyo toka kwangu wenye kuangamiza watamwendea.”—Yeremia 51:53.

  • Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • [Picha katika ukurasa wa 111]

      Babiloni mtafuta-anasa atashushwa chini kwenye vumbi

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki