Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Baba Mwenye Wana Waasi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 20 Isaya amalizia taarifa hii ya unabii, akisema: “Kama BWANA wa majeshi asingalituachia mabaki machache sana, tungalikuwa kama Sodoma, tungalifanana na Gomora.” (Isaya 1:9)c Hatimaye Yehova ataipa Yuda msaada dhidi ya Ashuru yenye nguvu. Tofauti na Sodoma na Gomora, Yuda haitafutiliwa mbali. Itaokoka.

      21. Baada ya Babiloni kuliharibu Yerusalemu, kwa nini Yehova ‘aliacha mabaki machache’?

      21 Zaidi ya miaka 100 baadaye, Yuda ilikuwa hatarini tena. Watu hawakuwa wamejifunza kutokana na nidhamu waliyopewa kupitia Ashuru. “Waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake.” Kwa hiyo, “ghadhabu ya BWANA [ikazidi] juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.” (2 Mambo ya Nyakati 36:16) Nebukadreza mtawala wa Babiloni alishinda Yuda, na wakati huo hakukubaki chochote “kama kibanda katika shamba la mizabibu.” Hata Yerusalemu liliharibiwa. (2 Mambo ya Nyakati 36:17-21) Na bado, Yehova ‘aliacha mabaki machache.’ Hata ingawa Yuda ilivumilia miaka 70 uhamishoni, Yehova alihakikisha kuwa taifa hilo laendelea na hasa nasaba ya Daudi, ambayo ingetokeza Mesiya aliyeahidiwa.

      22, 23. Katika karne ya kwanza, kwa nini Yehova ‘aliacha mabaki machache’?

      22 Katika karne ya kwanza, Israeli ilikabili mgogoro wake wa mwisho ikiwa watu wa agano la Mungu. Yesu alipojitokeza akiwa Mesiya aliyeahidiwa, taifa hilo lilimkataa, naye Yehova akawakataa. (Mathayo 21:43; 23:37-39; Yohana 1:11) Je, huo ulikuwa mwisho wa Yehova kuwa na taifa la pekee duniani? La. Mtume Paulo alionyesha kuwa Isaya 1:9 lingekuwa na utimizo mwingine tena. Akinukuu tafsiri ya Septuagint, aliandika hivi: “Kama vile Isaya alivyokuwa amesema wakati wa mbele: ‘Isingekuwa Yehova wa majeshi alikuwa ametuachia sisi mbegu, tungalikuwa kama Sodoma, nasi tungalifanywa kama vile Gomora.’”—Waroma 9:29.

      23 Mara hii wenye kuokoka walikuwa Wakristo watiwa-mafuta, waliomwamini Yesu Kristo. Mwanzoni kabisa, hao walikuwa Wayahudi waamini. Baadaye waamini wasio Wayahudi wakajiunga nao. Wote pamoja wakafanyiza Israeli mpya, “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16; Waroma 2:29) “Mbegu” hiyo iliokoka uharibifu wa mfumo wa mambo wa Kiyahudi mwaka wa 70 W.K. Kwa kweli, taifa la “Israeli wa Mungu” lingali nasi leo. Sasa mamilioni ya watu mmoja-mmoja wenye imani kutoka kwa mataifa, wanaofanyiza “umati mkubwa, ambao hakuna mtu [awezaye] kuuhesabu, kutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha” wamejiunga nalo.—Ufunuo 7:9.

      24. Wote wanaotaka kuokoka mgogoro mkuu wa mwanadamu wapaswa kuzingatia nini?

      24 Hivi karibuni ulimwengu huu utakabiliwa na vita ya Har–Magedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Ingawa huo utakuwa mgogoro mkubwa kuliko uvamizi wa Ashuru au wa Babiloni katika Yuda, mkubwa hata kuliko ukiwa uliosababishwa na Roma katika Yudea mwaka wa 70 W.K., kutakuwako wenye kuokoka. (Ufunuo 7:14) Basi, ni muhimu kama nini wote wafikirie kwa uzito maneno ya Isaya kwa Yuda! Hayo yaliokoa waaminifu wa wakati huo. Nayo yaweza kuokoa wenye imani leo.

  • Baba Mwenye Wana Waasi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • c Kichapo Commentary on the Old Testament, cha C. F. Keil na F. Delitzsch, chasema hivi: “Hapa pana kituo katika hotuba ya nabii huyo. Nafasi iliyoachwa kwenye maandishi kati ya mstari wa 9 na 10 yaonyesha hakika ya kwamba imegawanywa katika sehemu mbili mahali hapa. Mtindo huu wa kugawanya sehemu kubwa au ndogo, ama kwa kuacha nafasi au kwa kugawanya mstari, ni wa zamani kuliko ule wa alama za vokali na za lafudhi, nao hutegemea desturi bora ya zamani za kale.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki