Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wakati wa Nia Njema”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 22. Yehova anakaziaje kwamba hatawasahau watu wake kamwe?

      22 Sasa Isaya anaendelea kuripoti matamko rasmi ya Yehova. Anatabiri kwamba Waisraeli wahamishwa wataelekea kuchoka kabisa na kupoteza tumaini. Isaya anasema hivi: “Sayuni alisema, YEHOVA ameniacha, Bwana amenisahau.” (Isaya 49:14) Je, hii ni kweli? Je, Yehova amewaacha watu wake na kuwasahau? Akitenda kama msemaji wa Yehova, Isaya anaendelea kusema hivi: “Je! mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.” (Isaya 49:15) Hilo ni itikio lenye upendo kama nini kutoka kwa Yehova! Upendo wa Mungu kwa watu wake ni mkubwa kuliko ule wa mama kwa mtoto wake. Yeye anawafikiria daima waaminifu-washikamanifu wake. Anawakumbuka kana kwamba majina yao yamechorwa katika mikono yake: “Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima.”—Isaya 49:16.

      23. Paulo aliwatiaje moyo Wakristo watumainie kuwa Yehova hatawasahau?

      23 Katika barua yake kwa Wagalatia, mtume Paulo aliwahimiza Wakristo hivi: “Acheni tusife moyo katika kufanya lililo bora, kwa maana katika majira yapasayo tutavuna ikiwa hatuchoki kabisa.” (Wagalatia 6:9) Aliwaandikia Waebrania maneno haya ya kuwatia moyo: “Mungu si asiye mwadilifu ili asahau kazi yenu na upendo mlioonyesha kwa ajili ya jina lake.” (Waebrania 6:10) Hatupaswi kamwe kuhisi kwamba Yehova amewasahau watu wake. Kama Sayuni wa kale, Wakristo wana sababu nzuri ya kushangilia na kumngoja Yehova kwa subira. Yeye huyashika imara masharti ya agano lake na ahadi zake.

  • “Wakati wa Nia Njema”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 25. Nyakati za kisasa, Israeli wa kiroho alirudishwa katika hali gani?

      25 Maneno haya yana utimizo wa kisasa. Katika ile miaka migumu ya vita ya ulimwengu ya kwanza, Israeli wa kiroho alipatwa na kipindi cha ukiwa na utekwa. Lakini alirudishwa akaja kuwa katika paradiso ya kiroho. (Isaya 35:1-10) Inaweza kusemwa kwamba alifurahi sana, kama jiji lile ambalo Isaya alielezea habari zake, kwa kujikuta akimiminikwa na waabudu wengi wa Yehova wenye shangwe na utendaji mwingi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki