Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Msiwatumainie Wakuu”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 2 Yuda atajilaumu mwenyewe. Hana haki ya kudai kwamba uangamivu wake umetokea kwa sababu Yehova ametenda hila au amepuuza agano lake na taifa hilo. Muumba si mvunja-maagano. (Yeremia 31:32; Danieli 9:27; Ufunuo 15:4) Yehova anakazia uhakika huo kwa kuwauliza Wayahudi hivi: “Iko wapi hati ya talaka ya mama yenu, ambayo kwa hiyo naliachana naye?” (Isaya 50:1a) Chini ya Sheria ya Kimusa, mwanamume anayemtaliki mke wake ni lazima ampe hati ya talaka. Kisha mwanamke huyo anakuwa huru kuwa wa mwanamume mwingine. (Kumbukumbu la Torati 24:1, 2) Katika maana ya mfano, Yehova amempa Israeli, ule ufalme ulio dada ya Yuda, hati ya jinsi hiyo, lakini Yuda hakupewa.a Bado Yehova ndiye ‘mume na mmilikaji’ wa Yuda. (Yeremia 3:8, 14, NW) Yuda hayuko huru kamwe kuwa mwenzi wa mataifa ya kipagani. Uhusiano wa Yehova pamoja na Yuda utaendelea “mpaka Shilo [Mesiya] aje.”—Mwanzo 49:10, NW.

      3. Kwa nini Yehova ‘anawauza’ watu wake?

      3 Vilevile, Yehova anauliza Yuda hivi: “Nimewauza ninyi kwa nani katika watu wanaoniwia?” (Isaya 50:1b) Wayahudi hawatapelekwa katika utekwa Babiloni kulipia deni fulani ambalo Yehova amejiletea. Yehova si kama Mwisraeli maskini anayelazimika kumaliza madeni yake kwa kuwauza watoto wake kwa mkopeshaji. (Kutoka 21:7) Bali, Yehova anaonyesha sababu halisi itakayofanya watu wake wafanywe watumwa: “Ninyi mliuzwa kwa sababu ya maovu yenu; tena mama yenu ameachwa kwa sababu ya makosa yenu.” (Isaya 50:1c) Wayahudi ndio wamemwacha Yehova; siye amewaacha.

  • “Msiwatumainie Wakuu”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • a Katika mistari mitatu ya kwanza ya Isaya sura ya 50, Yehova anaeleza kwamba taifa la Yuda kwa ujumla ni mke wake, na wakaaji wake mmoja-mmoja ni watoto wake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki