Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je! Wewe Unabaki Ukiwa Safi Katika Kila Jambo?
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Novemba 1
    • Je! Wewe Unabaki Ukiwa Safi Katika Kila Jambo?

      “Jitengeni, Jitengeni, tokeni huko, msiguse kitu cho chote kichafu; tokeni katikati yake, endeleeni kuwa safi, ninyi ambao mnachukua vyombo vya Yehova.”—ISAYA 52:11, NW.

      1. (a) Amri ya kifalme iliruhusuje vyombo vya Yehova virudishwe Yerusalemu? (b) Baadhi ya vyombo hivyo vilikuwa vimechafuliwaje?

      KWA GHAFULA walikuwa huru—baada ya miaka 70 ya utumwa! Amri ya kifalme ya kama 538 K.W.K. iliruhusu hilo taifa la Kiyahudi kurudi na ‘kujenga nyumba ya Yehova, Mungu wa Israeli.’ (Ezra 1:2, 3) Halafu, tukio jingine lenye kushangaza: “Koreshi, mfalme [wa Uajemi] alivitoa vyombo vya nyumba ya Bwana [Yehova, NW] alivyokuwa amevileta Nebukadreza toka Yerusalemu.” (Ezra 1:7, 8) Miongoni mwa hizo vilikuwamo vile vyombo vitakatifu ambavyo Belshaza na watu wake wa cheo cha juu walikuwa wamevichafua katika ule usiku Babuloni ilipoanguka, wakivitumia kwa ufidhuli kusifu miungu isiyo ya kweli! (Danieli 5:3, 4) Sasa hao ambao hapo kwanza walikuwa uhamishoni wangeweza kurudisha vyombo hivi Yerusalemu vikatumiwe katika sifa ya Yehova!

      2. (a) Ni unabii gani wa Isaya ambao wenye kurudi wangekumbuka? Unabii huo ungehusu akina nani? (b) Ni kwa sababu gani walisihiwa wasiguse kitu cho chote kichafu?

      2 Walipojitayarisha kwa msisimuko kuondoka, Wayahudi hao wenye kurudi kwao bila shaka walikumbuka yale maneno ya nabii Isaya: “Jitengeni, jitengeni, tokeni huko, msiguse kitu cho chote kichafu; tokeni katikati yake, endeleeni kuwa safi, ninyi ambao mnachukua vyombo vya Yehova.” (Isaya 52:11, NW) Walawi, bila shaka, ndio waliofanya uchukuaji hasa wa vile vyombo. (Hesabu 1:50, 51; 4:15) Hata hivyo, Isaya alikuwa ametabiri kwamba wote wenye kurudi wangekuwa wachukuaji vyombo wenye heshima. Hivyo wote walikuwa na wajibu wa kuwa safi. Wao hawakuwa wawapore Wababuloni vitu vyote vyenye thamani kama walivyofanya Waisraeli wakati walipoondoka Misri. (Linganisha Kutoka 12:34-38.) Walikuwa sharti wawe huru na kusudio lo lote la kutaka vitu vya kimwili au la ubinafsi katika kurudi. Kwa habari ya “sanamumavi” za Babuloni, kugusa tu mojapo kungechafua!a (Yeremia 50:1, 2, NW) Ni kwa kuwa safi katika kila njia kwamba Wayahudi hawa wangeweza kutembea “ile Njia ya Utakatifu” kurudi Yerusalemu!—Isaya 35:8, 9.

      3. Ni nani leo wanaochukua “vyombo” vya Yehova? Ni kwa sababu gani ni shida sana kwao kubaki wakiwa safi?

      3 Mashahidi wa Yehova hali kadhalika lazima wawe safi wakiwa wachukuaji wa “vyombo” vya Yehova. Mtume Paulo alinakili maneno ya Isaya na akayatumia kwa Wakristo katika siku zake, akisema: “Na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.” (2 Wakorintho 6:17–7:1) Licha ya kuishi katika ulimwengu mchafu, sharti sisi tumenyane na mielekeo yetu ya kurithiwa yenye upungufu. (Mwanzo 8:21) Yeremia 17:9 inakumbusha sisi zaidi hivi: “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?” Wengine wanajidanganya wao wenyewe na wengine katika kuitikadi kwamba maisha zao ni safi na zinakubalika kwa Mungu, hali kwa kweli haziko hivyo. Wao wanazoea namna ya unafiki. Kwa hiyo lazima kila mmoja wetu ajiulize, ‘Je! mimi ninatia kila jitihada kuwa safi mbele za Yehova katika kila jambo? Kutusaidia sisi katika kufanya hivyo, acheni sasa sisi tukaze fikira kwenye pande nne za usafi.

  • Je! Wewe Unabaki Ukiwa Safi Katika Kila Jambo?
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Novemba 1
    • Je! Wewe Utabaki Ukiwa Safi?

      17, 18. Ni kwa sababu gani ni jambo la muhimu kusitawisha (a) usafi wa kimwili, (b) usafi wa kiakili, (c) usafi wa kiadili, na (d) usafi wa kiroho?

      17 Kwa hiyo mengi yanahusika katika kubaki tukiwa safi mbele za Yehova Mungu. Kuweka miili yetu, makao yetu, mavazi yetu, na Majumba ya Ufalme yetu yakiwa safi kwa jinsi ya kuonekana kunapamba ujumbe wa Ufalme wetu. Kuendelea kuwa safi kiakili kunasaidia sisi tukae tukiwa safi kiadili na kiroho. Hiyo inatutaka sisi tutii onyo la upole la Paulo kwenye Wafilipi 4:8 kuweka akili zetu juu ya mambo ambayo ni ya kweli, safi, na yenye staha!

      18 Sisi tunaweza pia kuthamini zaidi ya wakati wo wote uliotangulia kwamba lazima sisi tukae tukiwa safi kiadili katika maneno na matendo pia. Yehova anatuonya sisi waziwazi kwamba wale wanaojitia katika namna yo yote ya ukosefu wa adili hawatarithi kamwe Ufalme wa Mungu. (1 Wakorintho 6:9-11) Hata kama mambo hayo machafu yanaonekana kuwa yenye kupendeza jinsi gani, tukipanda kwa mwili, sisi tutavuna uharibifu kutoka kwa mwili. (Wagalatia 6:8) Kwa kumalizia, kuna lile jambo la kubaki tukiwa safi kiroho, kuwa safi kimafundisho. Usafi kama huo unasaidia sisi tudumishe usafi wa mioyo na akili zetu. Hivyo sisi sikuzote tunasukumwa kutafuta mawazo ya Mungu juu ya mambo—si yetu wenyewe.

      19. Ni nini kinachoweza kusaidia wapakwa-mafuta na “mkutano mkubwa” pia katika kubaki wakiwa safi katika mambo yote?

      19 Karibuni kisababishi chenyewe cha uchafu—Shetani Ibilisi—atatupwa, pamoja na mashetani wake, ndani ya lile shimo refu. Mpaka wakati huo, watumishi wote wa Yehova—wapakwa-mafuta na “mkutano mkubwa”—na wabaki wakiwa safi wakiwa wachukuaji wa vyombo vya Yehova. (Ufunuo 7:9, 13-15; 19:7, 8; 20:1-3, NW) Vita ni ya kuendelea na ngumu. Kumbuka, ingawa hivyo, kwamba Yehova anatoa kwa wingi “roho ya utakatifu” yake. (Warumi 1:4, NW) Tengenezo lake safi, pamoja na wazee walo, wanasimama tayari, pia, kusaidia sisi kwa kutoa shauri timamu la Kimaandiko. Tukiwa na msaada huo na kupiga moyo konde kwetu wenyewe, sisi tunaweza kubaki safi katika kila jambo!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki