-
Yehova Ahuisha Roho ya WanyenyekevuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
22. Yehova anatabiri wakati gani ujao kwa (a) wenye kutubu? (b) waovu?
22 Akitofautisha wakati ujao wa wale wanaotubu na wakati ujao wa wale wanaoendelea tu kufuata njia zao za uovu, Yehova anatangaza hivi: “Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; . . . nami nitamponya. Bali wabaya wanafanana na bahari iliyochafuka; maana haiwezi kutulia, na maji yake hutoa tope na takataka. Hapana amani kwa wabaya.”—Isaya 57:19-21.
-
-
Yehova Ahuisha Roho ya WanyenyekevuUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
24. (a) Ni nani wanaopata kujua amani ya Mungu, na matokeo ni nini? (b) Ni nani ambao hawapati kujua amani, na wanapatwa na matokeo gani?
24 Lo, Wayahudi wanatoa tunda la midomo lenye kusisimua kama nini wakati wanapoirudia nchi yao wakimwimbia Yehova sifa! Bila shaka wana shangwe ya kuijua amani ya Mungu, hata kama wako “mbali”—mwendo mrefu kutoka Yuda, wakiwa wangali wanangojea kurudi—au wakiwa “karibu,” yaani wakiwa tayari katika nchi yao. Lakini mambo ni tofauti kabisa kwa waovu! Waovu wowote wasioitikia nidhamu za Yehova, hata wawe akina nani, na hata wawe wapi, hawana amani hata kidogo. Wanachacha kama bahari iliyochafuka, wakiendelea kuzaa, si lile tunda la midomo, bali “tope na takataka” za baharini, uchafu wa kila aina.
-