-
Je! Wewe Utasema, “Mimi Nipo Hapa! Tuma Mimi”?Mnara wa Mlinzi—1987 | Oktoba 15
-
-
9. Ni jambo gani kuu lililohusika katika ujumbe wa Isaya?
9 Jambo hilo la kustaajabisha lililompata nabii lilimwongoza kupokea ule utume wa kuhubiri uliotajwa. (Isaya 6:8, 9) Lakini kwa sababu gani Isaya alipaswa kusema kwamba watu wangerudia-rudia kusikia lakini bado wasipate maarifa yo yote? Sauti ya Mungu iliongeza hivi: “Fanya moyo wa watu hawa uwe usiopokea mambo, na kufanya masikio yao yenyewe yawe yasiyoitikia mambo, na kugandamanisha pamoja macho yao yenyewe, kwamba wao wasione . . . na kwamba wao kwa kweli wasigeuke na kurejea kupata uponyi.” (Isaya 6:10, NW) Je! hilo linamaanisha kwamba Isaya, alipaswa kwa kutumia maneno yasiyofikiriwa vizuri au ukosefu wa busara aondolee mbali upendezi wa Wayahudi ili kwamba wao wangebaki wakiwa hawasikilizani na Yehova? Sivyo. Hicho kilikuwa kionyesho tu cha jinsi Wayahudi walio wengi wangeitikia hata kama Isaya angeitimiza kwa uaminifu na ukamili gani kazi ya kuhubiri ambayo yeye alikuwa amejitolea kwa kusema, “Mimi nipo hapa! Tuma mimi.”
10. (a) Kasoro ilikuwa wapi kwa habari ya watu kuwa kama vipofu na viziwi? (b) Isaya alimaanisha nini kwa kuuliza, “Kwa mudu mrefu jinsi gani?”
10 Kasoro ilikuwa ya watu wale. Ijapokuwa Isaya aliwaruhusu ‘wasikie tena na tena,’ wao hawakutaka kutwaa maarifa wala kupata ufahamu. Mungu alisema mapema kwamba walio wengi, kwa sababu ya mwelekeo wao wa ushupavu na usio wa kiroho, hawangeitikia. Wachache wangeweza. Lakini walio wengi zaidi wangekuwa vipofu kama kwamba macho yao yalikuwa yamegandamanishwa yakafungwa kwa gundi yenye nguvu kupita zote, ikiwa wewe unaweza kuwazia hilo. Je! hali mbaya hiyo ingeendelea kwa muda mrefu jinsi gani? Jambo hilo, badala ya ni miaka mingapi ambayo angetumikia, ndilo Isaya aliuliza kwa maneno haya: “Kwa muda mrefu jinsi gani, Ee Yehova?” Mungu alijibu: “Mpaka ile miji kwa kweli ibomoke iwe magofu, kuwa bila mkaaji.” Na hivyo ndivyo ilivyotukia, ingawa ni baada ya muda wa maisha ya Isaya. Wababuloni waliondoa binadamu wa duniani wakiacha Yuda ‘imefanywa magofu kuwa ukiwa.’—Isaya 6:11, 12; 2 Wafalme 25:1-26, NW.
-
-
Je! Wewe Utasema, “Mimi Nipo Hapa! Tuma Mimi”?Mnara wa Mlinzi—1987 | Oktoba 15
-
-
Mambo Makubwa Zaidi Yenye Kutimizwa
12. Ni msingi gani wa Kimaandiko uliopo wa kuita Yesu Isaya Mkubwa Zaidi?
12 Karne nyingi baada ya kifo cha Isaya, mmoja alikuja ambaye sisi tungeweza kumwita Isaya Mkubwa Zaidi—Yesu Kristo. Katika kuwako kwake kabla ya kuwa mwanadamu, yeye alikuwa amejitolea kutumwa na Baba yake kwenye dunia, ambako yeye angetia katika mahubiri yake mambo ambayo Isaya alikuwa ameandika. (Mithali 8:30, 31; Yohana 3:17, 34; 5:36-38; 7:28; 8:42; Luka 4:16-19; Isaya 61:1) Kwa kutaja wazi zaidi, Yesu alijihusianisha mwenyewe na Isaya sura ya 6 wakati alipokuwa akieleza sababu iliyofanya Yeye afundishe kama Yeye alivyofanya. (Mathayo 13:10-15; Marko 4:10-12; Luka 8:9,10) Jambo hilo lilifaa, kwa maana walio wengi wa Wayahudi ambao walisikia Yesu akisema hawakuwa na nia ya kukubali ujumbe wake na kutenda kulingana nao sawasawa tu na vile wale ambao walimsikia nabii Isaya akisema hawakuwa na nia ya kukubali ujumbe wake. (Yohana 12:36-43) Pia, katika 70 W.K., Wayahudi ambao walikuwa wamejifanya ‘vipofu na viziwi’ kwa ujumbe wa Yesu walipatwa na uharibifu kama ule wa 607 K.W.K. Tukio hilo katika karne ya kwanza lilikuwa dhiki juu ya Yerusalemu ‘ya namna ambayo haikuwa imetukia tangu mwanzo wa ulimwengu wala haingetukia tena.’ (Mathayo 24:21, NW) Hata hivyo, kama vile ambavyo Isaya alitoa unabii, baki, au “mbegu takatifu,” lilijizoeza imani. Hao walifanyizwa kuwa taifa la kiroho, yule “Israeli wa Mungu” mpakwa-mafuta.—Wagalatia 6:16.
13. Kwa sababu gani sisi tunaweza kutazamia utimizo mwingine bado wa Isaya 6?
13 Sasa sisi tunakuja kwenye utimizo mwingine wenye msingi wa Biblia wa Isaya sura ya 6. Kama ufunguo wa kufahamu utimizo huo, fikiria maneno ya mtume Paulo karibu na mwaka 60 W.K. Yeye alieleza sababu iliyofanya Wayahudi wengi ambao walisikia akisema katika Roma hawangekubali “ushuhuda [wake] kuhusu ufalme wa Mungu.” Sababu ilikuwa kwamba Isaya 6:9, 10 ilikuwa ikitimizwa tena. (Matendo 28:17-27) Je! hiyo inamaanisha kwamba baada ya Yesu kuiacha dunia, wanafunzi wake wapakwa-mafuta walipaswa kutekeleza utume unaolingana na ule wa Isaya? Ndiyo, kweli kweli!
14. Ni jinsi gani wanafunzi wa Yesu walikuwa sharti wafanye kazi kama ya Isaya?
14 Kabla ya Isaya Mkubwa Zaidi kupaa mbinguni, yeye alisema kwamba wanafunzi wake wangepokea roho takatifu na baada ya hapo ‘wangekuwa mashahidi wake katika Yerusalemu na katika Yudea yote na Samaria na kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.’ (Matendo 1:8, NW) Sawasawa na vile ile madhabahu ya dhabihu ilivyokuwa na kitu kilichohitajiwa ili kosa la Isaya liondoke, ndivyo dhabihu ya Yesu ilivyokuwa msingi wa kufanya kwamba wanafunzi wake wawe ‘wamelipiwa upatanisho wa dhambi yao yenyewe.’ (Walawi 6:12, 13; Waebrania 10:5-10; 13:10-15) Hivyo, Mungu angeweza kuwapaka mafuta kwa roho takatifu, na hiyo pia ingewatia nguvu wawe ‘mashahidi kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia. Wote wawili nabii Isaya na yule Isaya Mkubwa Zaidi walikuwa wametumwa kutangaza ujumbe wa Mungu. Vivyo hivyo wafuasi wapakwa-mafuta wa Yesu ‘walitumwa kutoka kwa Mungu kwa kuandamana pamoja na Kristo.’—2 Wakorintho 2:17 NW
-