-
Wachukuaji Nuru—Kwa Kusudi Gani?Mnara wa Mlinzi—1993 | Januari 15
-
-
16, 17. Yehova aliangazaje utukufu wake juu ya tengenezo lake lililo kama mwanamke katika 1914, na alimpa amri gani?
16 Kwa maneno yenye kuchochea moyo, Maandiko yanasimulia njia ambayo nuru ya kimungu inaenezwa kwa watu kila mahali. Isaya 60:1-3 linaloelekezwa kwa “mwanamke” wa Yehova au tengenezo lake la kimbingu la watumishi waaminifu-washikamanifu husema hivi: “Ondoka, [Ee mwanamke, NW] uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja, na utukufu wa BWANA [Yehova, NW] umekuzukia. Maana, tazama, giza litaifunika dunia, na giza kuu litazifunika kabila za watu; bali BWANA [Yehova, NW] atakuzukia wewe, na utukufu wake utaonekana juu yako. Na mataifa wataijilia nuru yako, na wafalme kuujia mwanga wa kuzuka kwako.”
-
-
Wachukuaji Nuru—Kwa Kusudi Gani?Mnara wa Mlinzi—1993 | Januari 15
-
-
20 Lakini ni kwa kusudi gani kwamba Yehova ameshughulika nao kwa njia hiyo? Kama vile yeye mwenyewe alivyosema kwenye Isaya 60:21, ni ili kwamba yeye ‘atukuzwe,’ jina lake lipate kuheshimiwa na wengine wavutwe kwake akiwa Mungu wa pekee wa kweli—ikitokeza faida ya milele kwao. Kupatana na hilo, katika 1931, waabudu hao wa Mungu wa kweli walikubali jina Mashahidi wa Yehova. Kama tokeo la kutoa kwao ushahidi, je! “wafalme” walivutwa kwenye nuru waliyoangaza, kama vile Isaya alivyotabiri? Ndiyo! Si watawala wa kisiasa wa dunia, bali idadi iliyobaki ya wale walio katika mstari wa kutawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo katika Ufalme wake wa kimbingu. (Ufunuo 1:5, 6; 21:24) Namna gani “mataifa”? Je! wao wamevutwa kwenye nuru hiyo? Bila shaka ndivyo! Hakuna taifa moja la kisiasa ambalo limevutwa, bali mkutano mkubwa wa watu kutoka katika mataifa hayo yote wamechukua msimamo wao upande wa Ufalme wa Mungu, na wanatazamia kwa hamu ukombozi ili kuingia ulimwengu mpya wa Mungu. Utakuwa ulimwengu mpya kwelikweli ambamo uadilifu utaenea.—2 Petro 3:13; Ufunuo 7:9, 10.
-