Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matokeo ya Kuhubiri​—“Mashamba . . . Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa”
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
    • 15. Maneno yaliyo kwenye Isaya 60:5, 22 yametimizwaje? (Ona pia masanduku “Yehova Alifanya Iwezekane,” kwenye ukurasa wa 93, na “Jinsi Ambavyo ‘Mnyonge’ Amekuwa ‘Taifa Lenye Nguvu,’” kwenye ukurasa wa 96-97.)

      15 Miaka 800 hivi kabla Yesu hajatoa mifano hiyo, Yehova, kupitia nabii Isaya, alitabiri kwa lugha rahisi kuhusu kuenea kwa mavuno ya kiroho katika siku zetu, na shangwe ambayo ingesababishwa na kazi hiyo ya kuvuna.c Yehova anaeleza kwamba watu “kutoka mbali” wanamiminika katika tengenezo lake. Akizungumza na “mwanamke,” ambaye leo anawakilishwa na watiwa-mafuta ambao wangali duniani, anasema hivi: “Utaona na hakika ung’ae, na moyo wako kwa kweli utatetemeka na kupanuka, kwa sababu mali za bahari zitajielekeza kwako; mali za mataifa zitakuja kwako.” (Isa. 60:1, 4, 5, 9) Maneno hayo ni kweli kabisa! Leo, watumishi wa Yehova ambao wamemtumikia kwa muda mrefu, kwa kweli wanang’aa kwa shangwe wanapoona jinsi ambavyo idadi ya wahubiri wa Ufalme katika nchi zao imeongezeka kutoka watu wachache tu hadi maelfu ya watu.

  • Matokeo ya Kuhubiri​—“Mashamba . . . Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa”
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
    • c Kwa habari zaidi kuhusu unabii huu wenye kupendeza, ona kitabu Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote II, ukurasa wa 303-320.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki