-
Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni PoteUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
13. Nyakati za kisasa, “wana” na “binti” ni akina nani, na “utajiri wa mataifa” ni akina nani?
13 Lo, andiko la Isaya 60:4-9 linatoa ufafanuzi ulio wazi kama nini kuhusu mpanuko ambao umetukia ulimwenguni pote tangu “mwanamke” wa Yehova aanze kuangaza nuru katikati ya giza la ulimwengu huu! Kwanza wakafika “wana” na “binti” za Sayuni wa kimbingu, wale waliokuja kuwa Wakristo watiwa-mafuta. Mwaka wa 1931, walijitambulisha peupe kuwa Mashahidi wa Yehova. Halafu wingu la watu watiifu, ambao ndio “utajiri wa mataifa” na “wingi wa bahari,” likafanya haraka kujiunga na ndugu za Kristo waliobaki.b Leo watumishi wote hawa wa Yehova wanaotoka pembe nne za dunia na kutoka hali zote za maisha wanajiunga na Israeli wa Mungu kumsifu Bwana wao Mwenye Enzi Kuu, Yehova, na kukweza jina lake kuwa ndilo tukufu zaidi katika ulimwengu mzima.
-
-
Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni PoteUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
b Ingawa Wakristo fulani wenye bidii na wenye tumaini la kidunia walishirikiana na Israeli wa Mungu kabla ya mwaka wa 1930, idadi yao ilianza kuongezeka sana katika miaka ya 1930.
-