-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
17. (a) Washirika wa Israeli wa Mungu wataitwaje? (b) Ni dhabihu gani moja tu inayohitajiwa ili kuwe na msamaha wa dhambi?
17 Namna gani juu ya Israeli wa Mungu? Yehova anawaambia hivi, kupitia Isaya: “Bali ninyi mtaitwa makuhani wa BWANA; watu watawaiteni wahudumu wa Mungu wetu; mtakula utajiri wa mataifa, na kujisifia utukufu wao.” (Isaya 61:6) Katika Israeli ya kale, Yehova alifanya uandalizi ili ukuhani wa Kilawi utoe dhabihu kwa niaba ya makuhani wenyewe na Waisraeli wenzao. Hata hivyo, mwaka wa 33 W.K., Yehova alikoma kutumia ukuhani wa Kilawi na kuanzisha mpango mzuri zaidi. Aliukubali uhai mkamilifu wa Yesu kuwa dhabihu kwa ajili ya dhambi za wanadamu. Tangu wakati huo, hakuna dhabihu nyingine yoyote ambayo imehitajiwa. Dhabihu ya Yesu ina nguvu za kutumika daima dawamu.—Yohana 14:6; Wakolosai 2:13, 14; Waebrania 9:11-14, 24.
18. Israeli wa Mungu wanakuwa ukuhani wa aina gani, na wana utume gani?
18 Basi, washirika wa Israeli wa Mungu ni ‘makuhani wa Yehova’ jinsi gani? Akiwaandikia Wakristo wenzake watiwa-mafuta, mtume Petro alisema hivi: “Nyinyi ni ‘jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu kwa ajili ya miliki ya pekee, kwamba mpate kutangaza kotekote sifa bora kabisa’ za yeye aliyewaita nyinyi kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.” (1 Petro 2:9) Kwa hiyo, wakiwa kikundi, Wakristo watiwa-mafuta wanakuwa ukuhani wenye utume hususa: kuyaambia mataifa juu ya utukufu wa Yehova. Wanapaswa kuwa mashahidi wake. (Isaya 43:10-12) Muda wote wa siku za mwisho, Wakristo watiwa-mafuta wameutimiza utume huo muhimu kwa uaminifu. Matokeo ni kwamba, sasa mamilioni ya watu wanashirikiana nao katika kazi ya kutoa ushahidi juu ya Ufalme wa Yehova.
19. Wakristo watiwa-mafuta watapendelewa kufanya utumishi gani?
19 Zaidi ya hilo, washirika wa Israeli wa Mungu wana tazamio la kutumikia wakiwa makuhani kwa njia nyingine. Wakiisha kufa, wanafufuliwa mbinguni wakiwa roho wasioweza kufa. Licha ya kutumikia wakiwa watawala pamoja na Yesu katika Ufalme wake huko, wanatumikia pia wakiwa makuhani wa Mungu. (Ufunuo 5:10; 20:6) Katika hali hiyo, watapendelewa kutumia faida za dhabihu ya fidia ya Yesu kuelekea wanadamu waaminifu duniani. Katika njozi ya mtume Yohana iliyoandikwa katika Ufunuo sura ya 22, wanatajwa tena kuwa “miti.” “Miti” yote 144,000 inaonwa ikiwa mbinguni, ikitokeza ‘mazao kumi na mawili ya matunda, ikitoa matunda yake kila mwezi. Na majani ya hiyo miti yalikuwa ya kuponya mataifa.’ (Ufunuo 22:1, 2) Lo, huo ni utumishi wa kikuhani ulio mzuri kama nini!
-
-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
a Isaya 61:5 yaweza kuwa ilitimizwa nyakati za kale, kwa kuwa watu wasio Wayahudi waliambatana na Wayahudi wa asili wakati wa kurudi kwao Yerusalemu, na inaelekea walisaidia kuirudishia nchi hali yake ya kwanza. (Ezra 2:43-58) Hata hivyo, kuanzia mstari wa 6 unabii unaelekea kutumika kuhusu Israeli wa Mungu peke yake.
-