Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Wapewa “Jina Jipya” na Yehova

      6. Yehova ana lengo gani kuhusu Sayuni?

      6 Yehova ana lengo gani kuhusu Sayuni, “mwanamke” wake wa kimbingu, aliyewakilishwa na Yerusalemu la kale? Anasema hivi: “Mataifa wataiona haki yako [“Ee mwanamke,” “NW”], na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha BWANA.” (Isaya 62:2) Wakati Waisraeli wanapotenda uadilifu, mataifa yanalazimika kuangalia kwa makini. Hata wafalme wanalazimika kukubali kwamba Yehova anatumia Yerusalemu na kwamba utawala wowote walio nao si kitu ukilinganishwa na Ufalme wa Yehova.—Isaya 49:23.

      7. Jina jipya la Sayuni linamaanisha nini?

      7 Sasa Yehova anampa Sayuni jina jipya ili kuthibitisha kwamba hali yake imebadilika. Jina hilo jipya linamaanisha hali yenye baraka na cheo chenye heshima kinachofurahiwa na watoto wa kidunia wa Sayuni kuanzia mwaka wa 537 K.W.K.a Linaonyesha kwamba Yehova anamkubali Sayuni kuwa mali yake. Leo, Israeli wa Mungu wanasisimuka kuwa kipenzi cha Yehova kwa njia hiyo, na wale kondoo wengine wanashangilia pamoja nao.

  • “Jina Jipya”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • a Katika unabii wa Biblia, “jina jipya” linaweza kumaanisha cheo kipya au pendeleo jipya.—Ufunuo 2:17; 3:12.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki