-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
13, 14. (a) Nyakati za kale, Yerusalemu linakuwaje jiji lenye usalama? (b) Nyakati za kisasa, Sayuni amekuwaje “sifa duniani”?
13 Jina jipya la mfano ambalo Yehova amewapa watu wake huwafanya wahisi usalama. Wanajua kwamba yeye huwakubali na kwamba wao ni miliki yake. Sasa Yehova anatumia mfano tofauti na kuongea na watu wake kana kwamba anaongea na jiji lenye kuta: “Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha [“kumtaja,” “NW”] BWANA, msiwe na kimya; wala msimwache akae kimya, mpaka atakapoufanya imara Yerusalemu, na kuufanya kuwa sifa duniani.” (Isaya 62:6, 7) Katika wakati wa Yehova, baada ya mabaki waaminifu kutoka Babiloni, Yerusalemu linakuwa “sifa duniani”—jiji lenye kuta za kuwapa wakaaji wake usalama. Mchana na usiku, walinzi katika kuta hizo wako macho kuhakikisha kwamba jiji lina usalama, na kuwapasha wakaaji wake habari za kuwaonya.—Nehemia 6:15; 7:3; Isaya 52:8.
14 Nyakati za kisasa Yehova amewatumia walinzi wake watiwa-mafuta kuwaonyesha watu watiifu njia ya kupata uhuru kutoka kwenye utumwa wa dini ya uwongo. Watu hao wamealikwa waje ndani ya tengenezo lake, ambamo wanalindwa wasipatwe na uchafu wa kiroho, mavutano ya kutomhofu Mungu, na ili wasichukiwe na Yehova. (Yeremia 33:9; Sefania 3:19) Jamii ya mlinzi, yaani yule “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” inatimiza fungu muhimu sana la kutoa ulinzi huo, kwani inaandaa ‘chakula cha kiroho kwa wakati ufaao.’ (Mathayo 24:45-47) Kwa kufanya kazi na jamii ya mlinzi, ule “umati mkubwa” pia hushiriki sehemu ya maana katika kufanya Sayuni awe “sifa duniani.”—Ufunuo 7:9.
-
-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
16. Ni jinsi gani watumishi wa Yehova ‘wasivyomwacha akae kimya’?
16 Watumishi wa Yehova wanatiwa moyo kusali bila kukoma, kumwomba Mungu ‘mapenzi yake yatendeke, kama ilivyo katika mbingu, pia juu ya dunia.’ (Mathayo 6:9, 10; 1 Wathesalonike 5:17) Wanahimizwa hivi: “Msimwache [Yehova] akae kimya” mpaka awatimizie tamaa zenu na matumaini yanayohusiana na kurudishwa kwa ibada ya kweli. Yesu alikazia uhitaji wa kusali daima, akawahimiza wafuasi wake ‘kumpaazia Mungu kilio mchana na usiku.’—Luka 18:1-8.
-