-
Yehova Ajifanyia Jina MaridadiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
14. Sasa Isaya anatoa vikumbusha gani vinavyofaa?
14 Nyakati zilizopita, Wayahudi waliacha upesi kuyathamini mambo ambayo Yehova aliwafanyia. Basi, inafaa kwamba Isaya anawakumbusha ni kwa nini Yehova alifanya mambo hayo. Isaya anatangaza hivi: “Nitautaja wema wa BWANA, sifa za BWANA kwa yote aliyotukirimia BWANA; na wingi wa wema wake kwa nyumba ya Israeli, aliowakirimia kwa rehema zake, na kwa wingi wa wema [“fadhili za upendo,” “NW”] wake. Maana alisema, Hakika ndio watu wangu hawa, wana wasio na hila; akawa Mwokozi wao. Katika mateso yao yote yeye aliteswa, na malaika wa uso wake [“mjumbe wake binafsi,” “NW”] akawaokoa; kwa mapenzi yake, na huruma zake, aliwakomboa mwenyewe; akawainua, akawachukua siku zote za kale.”—Isaya 63:7-9.
-
-
Yehova Ajifanyia Jina MaridadiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
16. (a) Yehova alikuwa na maoni gani alipofanya agano lake na Israeli? (b) Mungu anashughulikaje na watu wake?
16 Baada ya lile tukio la Kutoka, Yehova aliwaleta Israeli kwenye Mlima Sinai, akawapa ahadi hii: “Ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu . . . nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.” (Kutoka 19:5, 6) Je, Yehova alikuwa mdanganyifu kwa kuahidi hivyo? Sivyo, kwa maana Isaya anafunua kwamba Yehova alijiambia hivi yeye mwenyewe: “Hakika ndio watu wangu hawa, wana wasio na hila.” Msomi mmoja anatoa maoni haya: “Neno hili ‘hakika’ halitumiwi kimamlaka ili kujionyesha kuwa na enzi kuu ya kujitawala wala kuonyesha uwezo wa kujua mambo kimbele: bali limetumiwa kuonyesha tumaini na uhakika wenye upendo.” Ndiyo, Yehova alifanya agano lake kwa nia safi, akiwa na tamaa ya moyo mweupe ya kuwasaidia watu wake wafanikiwe. Ingawa walikuwa na mapungufu ya wazi, yeye alionyesha kwamba anawaamini. Ni vizuri kama nini kuabudu Mungu anayewaamini waabudu wake! Leo, wazee wanapoonyesha kuwa hata wao wanaamini kwamba kwa msingi watu wa Mungu ni wema, hiyo husaidia sana kuwaimarisha wale waliowekwa chini ya uangalizi wao.—2 Wathesalonike 3:4; Waebrania 6:9, 10.
-