-
Je, Yesu Alikuwa Akizungumza Kuhusu Moto wa Mateso?Mnara wa Mlinzi—2008 | Juni 15
-
-
Hata hivyo, linganisha maneno ya Yesu na mstari wa mwisho wa unabii wa Isaya.b Je, si wazi kwamba Yesu alikuwa akirejelea mstari huo katika Isaya sura ya 66? Inaelekea nabii huyo anazungumza kuhusu kwenda nje ya “Yerusalemu mpaka kandokando ya Bonde la Hinomu (Gehena), ambako wakati fulani dhabihu za wanadamu zilitolewa (Yer. 7:31) na mwishowe likawa sehemu ya kutupia takataka za jiji hilo.” (The Jerome Biblical Commentary) Lugha ya mfano inayotumiwa kwenye Isaya 66:24 haionyeshi kamwe kwamba watu wanateswa katika moto; andiko hilo linazungumza kuhusu mizoga. Katika andiko hilo, funza ndio wanaosemwa kuwa hawafi, bali si wanadamu walio hai au nafsi zisizoweza kufa. Hivyo basi, Yesu alimaanisha nini?
Ona maelezo kuhusu Marko 9:48 katika Buku la 2 la kichapo kimoja cha Kikatoliki (El evangelio de Marcos. Análisis lingüístico y comentario exegético): “Maneno hayo yanatoka katika Isaya (66,24). Hapo nabii anataja mambo mawili kuonyesha jinsi miili ya watu waliokufa ilivyoharibika: ilioza na kuteketezwa . . . Kutaja funza pamoja na moto katika maandishi hayo kunakazia wazo la uharibifu. . . . Nguvu hizo mbili za kuharibu zinaelezwa kuwa za kudumu (‘hazizimwi, hazifi’): hakuna njia yoyote ya kuziepuka. Katika maana hii ya mfano, ni funza na moto tu ndivyo haviharibiwi, bali si watu, na vinaharibu kabisa kila kitu kilicho katika uwezo wake. Kwa hiyo, huo si ufafanuzi wa mateso ya milele, lakini wa uharibifu wa milele. Wale wanaopata uharibifu huo hawafufuliwi kamwe, kifo chao ni cha milele. Hivyo basi, moto unafananisha kuharibiwa kabisa.”
-
-
Je, Yesu Alikuwa Akizungumza Kuhusu Moto wa Mateso?Mnara wa Mlinzi—2008 | Juni 15
-
-
b “Kwa kweli wataenda na kuitazama mizoga ya wale watu waliokuwa wakinikosea; kwa maana funza walio juu yao hawatakufa na moto wao hautazimwa, nao watakuwa chukizo kwa wanadamu wote.”—Isa. 66:24.
-