-
Ni Nini Hutokea Tunapokufa?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
2. Kwa nini ni muhimu kujua ukweli kuhusu kifo?
Watu wengi wanaogopa kifo, hata wanawaogopa watu waliokufa! Lakini mambo ambayo Biblia inasema kuhusu kifo yanaweza kukufariji. Yesu alisema: “Kweli itawaweka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Baadhi ya dini hufundisha kwamba mtu anapokufa nafsi yake huendelea kuishi, lakini Biblia haifundishi hivyo. Basi, hakuna mtu anayeteseka baada ya kufa. Pia, kwa sababu watu waliokufa hawajui jambo lolote, hawawezi kutudhuru. Hivyo, hatuhitaji kuwatuliza au kuwaabudu watu waliokufa, wala kusali kwa ajili yao.
Watu fulani hudai kwamba wana uwezo wa kuwasiliana na watu waliokufa. Lakini hilo haliwezekani. Kama tulivyojifunza, “waliokufa hawajui jambo lolote kamwe.” Wale wanaofikiri wanawasiliana na wapendwa wao waliokufa, inawezekana kwamba wanawasiliana na roho waovu ambao hujifanya kuwa watu waliokufa. Kwa hiyo, kujua ukweli kuhusu kifo hutulinda dhidi ya roho waovu. Yehova anatuonya kwamba tusijaribu kuwasiliana na watu waliokufa kwa sababu anajua tukiwasiliana na roho waovu tutapata madhara.—Soma Kumbukumbu la Torati 18:10-12.
-
-
Ni Nini Hutokea Tunapokufa?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
4. Ni muhimu kujua ukweli kuhusu kifo
Kujua ukweli kuhusu kifo, hutusaidia tusiwaogope watu waliokufa. Soma Mhubiri 9:10, kisha mzungumzie swali hili:
Je, watu waliokufa wanaweza kutudhuru?
Ukijifunza ukweli ulio katika Biblia kuhusu watu waliokufa, hutaamini uwongo wa kwamba tunapaswa kuwatuliza au kuwaabudu watu waliokufa. Soma Isaya 8:19 na Ufunuo 4:11, kisha mzungumzie swali hili:
Unafikiri Yehova anahisije kuhusu mtu anayeabudu au kutafuta msaada kutoka kwa watu waliokufa?
Ukweli kuhusu kifo unatuweka huru kutoka kwenye desturi zisizompendeza Yehova
-