-
Ole Wao Waasi!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
17, 18. Mifumo ya kisheria na ya utawala ya Israeli ina ufisadi gani?
17 Kisha Yehova akaza jicho lake lenye kuhukumu juu ya waamuzi wafisadi wa Israeli na maofisa wengine. Wao hutumia vibaya mamlaka yao kwa kuwapora maskini na waliotaabishwa ambao huwaendea ili kutafuta haki. Isaya asema: “Ole wao wawekao amri zisizo za haki, na waandishi waandikao maneno ya ushupavu; ili kumpotosha mhitaji asipate haki yake, na kuwanyang’anya maskini wa watu wangu haki yao; ili wajane wawe mateka yao, na kuwafanya yatima waliofiwa na baba zao kuwa mawindo yao!”—Isaya 10:1, 2.
18 Sheria ya Yehova hukataza namna zote za ukosefu wa haki: “Msitende yasiyo haki katika hukumu, usimpendelee mtu maskini, wala kumstahi mwenye nguvu.” (Mambo ya Walawi 19:15) Maofisa hao waipuuza sheria hiyo, na kujiwekea “amri zisizo za haki” ili kuhalalisha wizi ulio wazi na wenye ukatili sana—kutwaa mali chache za wajane na mayatima. Kwa wazi, miungu vipofu ya Israeli haioni ukosefu huo wa haki, lakini Yehova auona. Kupitia Isaya, Yehova sasa awakazia fikira waamuzi hao waovu.
-
-
Ole Wao Waasi!Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
[Picha katika ukurasa wa 141]
Yehova atawatoza hesabu wale wanaowaonea wengine
-