Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Msiogope Ashuru
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Mfalme Ahazi ajaribu kupata usalama kwa kutafuta msaada kwa Ashuru. Nabii Isaya atabiri kuwa wakati fulani baadaye, waliosalia katika nyumba ya Israeli hawatafuatia tena kamwe mwendo huo wa kipumbavu. Isaya 10:20 yasema kwamba “watamtegemea BWANA [“Yehova,” NW], Mtakatifu wa Israeli, kwa kweli.” Hata hivyo, mstari wa 21 waonyesha kuwa ni wachache tu watakaofanya hivyo: “Mabaki . . . watamrudia Mungu.” Hilo latukumbusha Shear-yashubu, mwana wa Isaya, aliye ishara katika Israeli na ambaye jina lamaanisha “Mabaki Wachache Tu Ndio Watakaorudi.” (Isaya 7:3) Mstari wa 22 katika sura ya 10 waonya juu ya kuja kwa “kuangamiza” ambako kumekusudiwa. Kuangamiza huko kutakuwa kwa haki kwa sababu ni adhabu inayofaa kwa watu waasi. Tokeo ni kwamba, kutoka kwa taifa lenye wakazi wengi “kama mchanga wa pwani,” ni mabaki wachache tu watakaorudi. Mstari wa 23 waonya kuwa angamizo hilo linalokuja litaathiri nchi nzima. Yerusalemu halitaachwa salama mara hii.

  • Msiogope Ashuru
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Unabii katika Isaya 10:20-23 ulikuwa na utimizo mwingine zaidi katika karne ya kwanza, kama ionyeshwavyo katika Waroma 9:27, 28. (Linganisha Isaya 1:9; Waroma 9:29.) Paulo aeleza kwamba kwa njia ya kiroho, “mabaki” ya Wayahudi ‘walimrudia’ Yehova katika karne ya kwanza W.K., kwa vile ni Wayahudi waaminifu wachache waliokuja kuwa wafuasi wa Yesu Kristo na kuanza kumwabudu Yehova “kwa roho na kweli.” (Yohana 4:24) Baadaye wasio Wayahudi wenye kuamini wakajiunga nao, wakifanyiza taifa la kiroho, “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Katika pindi hiyo, maneno ya Isaya 10:20 yalitimizwa: Taifa lililojiweka wakfu kwa Yehova halikumwacha “tena” kamwe ili kutegemezwa na binadamu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki