-
Yesu KristoUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
“Mshauri wa Ajabu.” Kuhani alikuwa na daraka la kuelimisha watu juu ya sheria na mapenzi ya Mungu. (Mal 2:7) Pia, akiwa Masihi wa kifalme, ‘tawi kutoka katika kisiki cha Yese baba ya Daudi,’ lililotabiriwa, Yesu alipaswa kudhihirisha ‘roho ya Yehova katika hekima, shauri, nguvu, ujuzi, pamoja na kumwogopa Yehova.’ Hivyo watu wenye kumwogopa Mungu ‘wangepata shangwe kupitia yeye.’ (Isa 11:1-3) Hekima isiyo na kifani inayopatikana katika mafundisho ya Yesu, ambaye alikuwa ni “mkuu kuliko Sulemani” (Mt 12:42), ndio mojawapo ya uthibitisho wenye nguvu zaidi kwamba kwelikweli yeye alikuwa Mwana wa Mungu na kwamba masimulizi ya zile Injili hayawezi kuwa yalitokezwa na akili au mawazo ya wanadamu wasiokamilika.
-
-
RohoUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Akiwa ndiye Mfalme wa Kimesiya, Kristo Yesu ana “roho ya hekima na ya uelewaji, roho ya shauri na ya nguvu, roho ya ujuzi na ya kumwogopa Yehova.” (Isa 11:1, 2; 42:1-4; Mt 12:18-21) Kani hiyo ambayo ni kwa ajili ya uadilifu inadhihirishwa na matumizi yake ya kani ya utendaji ya Mungu, au roho, katika kuongoza kutaniko la Kikristo duniani, kupitia kuwekwa kwake rasmi na Mungu, Yesu akiwa ndiye Kichwa chalo, Mwenyeji, na Bwana. (Kol 1:18; Yuda 4) Kama “msaidizi,” sasa roho hiyo iliwapa uelewaji ulioongezeka wa mapenzi na kusudi la Mungu na kuwafunulia Neno la Mungu la kinabii. (1Ko 2:10-16; Kol 1:9, 10; Ebr 9:8-10) Walitiwa nishati ya kutumikia wakiwa mashahidi katika dunia yote (Lu 24:49; Mdo 1:8; Efe 3:5, 6); walipewa ‘zawadi za roho’ za kimuujiza, zikawawezesha kusema katika lugha za kigeni, kutoa unabii, kuponya, na kutenda shughuli nyingine ambazo zingewawezesha kutangaza habari njema na pia kuwa uthibitisho wana utume na tegemezo la kimungu.—Ro 15:18, 19; 1Ko 12:4-11; 14:1, 2, 12-16; linganisha Isa 59:21; ona GIFTS FROM GOD (Gifts of the Spirit).
-