-
Kwa Nini Tunapaswa Kuhofu Mungu?Mnara wa Mlinzi—1989 | Januari 1
-
-
Ikiwa ndivyo, fikiria maana ya kuwa Mkristo. Kulingana na Biblia, kuwa Mkristo kunahusisha ndani kufuata kwa ukaribu katika hatua za nyayo za Yesu Kristo. (1 Petro 2:21) Sasa, ingawa hakuna shaka kwamba Yesu alipenda Mungu, Biblia inaonyesha wazi sana kwamba yeye alihofu Mungu pia.Isaya, akinena kwa unabii juu ya Yesu, alisema kwamba angekuwa na “roho ya maarifa na ya hofu kwa Yehova.” (Isaya 11:2, NW) Ingawa hivyo, jambo la kupendeza ni kwamba hofu hiyo haikuwa himila nzito juu ya Yesu. Haitupasi kuifikiria kuwa kama vile mtoto anavyohofu baba mkatili au vile idadi ya watu inavyoogofywa na mtawala mwonevu. Kwa uhakika, Isaya alitoa unabii huu pia juu ya Yesu: Yeye ataona shangwe katika kuhofu Yehova.” (Isaya J.l:3, NW) Wewe unaweza kuonaje shangwe juu ya kuogopa mtu fulani?
Uhakika ni kwamba, katika Biblia neno “hofu” lina maana mbalimbali. Kuna ile hofu au mtetemo wa kimwili tunaohisi wakati mtu fulani anapotaka kutudhuru. Hivyo, majeshi ya Kiisraeli ‘waliogopa sana’ Goliathi. (1 Samweli 17:23, 24) Halafu kuna ile hofu ya mambo ya kugutusha yasiyotarajiwa au yasiyojulikana, kama ile aliyohisi Zekaria alipokabiliwa kwa ghafula na malaika wa Yehova hekaluni. (Luka 1:11, 12) Hata hivyo, hofu ambayo Yesu alihisi kwa Baba yake haikuwa kama yoyote ya hizo.
Badala ya hivyo, maneno ya awali ya Kiebrania na Kigiriki yanayotumiwa katika Biblia kuhusu “hofu” huwa mara nyingi yanarejezea kicho kingi sana na staha kubwa mno kwa Mungu. Hiyo ndiyo hofu ya kumcha Mungu aliyokuwa nayo Yesu na ambayo malaika yule alikuwa akimtia moyo kila mtu leo aisitawishe. Hiyo staha kubwa mno, au hofu, hutia mizizi katika moyo wetu wakati tunapotafakari juu ya uweza na nguvu za Yehova na kuzilinganisha na uduni wetu ulio kamili. Hiyo huwa inakua wakati sisi tunapofikiria sana kazi zake zenye uweza, na inakuzwa pia kwa kukumbuka katika sala uhakika wa kwamba yeye ndiye Hakimu Mkuu Kupita Wote, mwenye nguvu za kutolea uhai na vilevile kuadhibu kwa kifo cha milele.
-
-
Kwa Nini Tunapaswa Kuhofu Mungu?Mnara wa Mlinzi—1989 | Januari 1
-
-
Kwenye Zaburi 19:9, W, tunafundishwa hivi: “Hofu kwa Yehova ni yenye utakato, ikisimama milele. Maamuzi ya hukumu za Yehova ni ya kweli; yamethibitika kabisa kuwa ya uadilifu.” Kwa hiyo hakuna jambo lolote la mwelekeo hasi kuhusu hofu kwa Mungu. Hiyo ina utakato na himaya na hufanya mtumishi wa Mungu awe mwenye imara kuliko adui zake. Kama Yesu, Mkristo hupata uradhi katika hofu hiyo kwa njia ile ile ambayo yeye huona shangwe juu ya baraka nyingine zote kutoka kwa Yehova.—Isaya 11:3.
-