Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Bustani ya Edeni Yarudishwa—Duniani Pote
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
    • 6, 7. (a) Ni kwa sababu gani viumbe wanyama havitakuwa tisho kwa wanadamu? (b) Ni unabii gani kuhusu hilo utakaokuwa na utimizo halisi?

      6 Viumbe wanyama havitadhuru au kuwa tisho kwa wakaaji wa Paradiso iliyorudishwa. Mungu atarudishia viumbe wa hali ya chini kadiri yo yote ya kuwaogopa wanadamu iliyopotea. Hivyo tunaweza kutazamia yale maelezo yenye kupendeza ya maisha ya wanyama yaliyoandikwa kwenye Isaya 11:6-9 yawe na utimizo halisi wakati wa Utawala wa Mileani wa “Mwana-Mfalme wa Amani”:

      7 “Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza. Ng’ombe na dubu watalisha pamoja; watoto wao watalala pamoja; na simba atakula majani kama ng’ombe. Na mtoto anyonyaye atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa atatia mkono wake katika pango la fira. Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua [Yehova], kama vile maji yanavyoifunika bahari.”

      8. Ni nini kinachomaanishwa na usemi wa kiunabii kwamba “mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka”?

      8 Lingekuwa jambo lisilopatana kwa Mungu kuongoza unabii kama huo uwe na maana ya kiroho tu bila kuonyesha mambo hayo katika maisha halisi ya kidunia. Hali moja na hiyo, Isaya 65:25 hutuambia hivi: “Mbwa-mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani kama ng’ombe; na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka.” Je! hilo linamaanisha kuangamizwa kabisa kwa jamaa ya nyoka isiwepo katika bustani ya Edeni yenye kuenea dunia yote? Hapana, usemi wa kiunabii kwamba “mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka” unamaanisha kwamba washiriki wa jamaa ya mtambaazi hawatakuwa hatari tena kamwe kwa maisha na afya njema ya viumbe wanadamu. Wao watalazimika kutambua kwamba wanadamu ndio mabwana zao walio na utawala juu ya kila kiendacho juu ya dunia, kama vile ilivyokuwa kwa habari ya Adamu katika bustani ya Edeni wakati alipowapa wanyama wote majina bila woga.—Mwanzo 2:19, 20; Hosea 2:18.

  • Bustani ya Edeni Yarudishwa—Duniani Pote
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
    • 11. Ni badiliko gani katika lugha litakalotukia, na hilo litakuwa na matokeo gani juu ya wanadamu?

      11 Je! Paradiso hiyo ya duniani pote itaharibiwa na mchafuko wa kuwa na lugha nyingi? Hapana, kwa sababu yule “Mwana-Mfalme wa Amani” vilevile anaitwa “Mungu Mwenye Nguvu.” (Isaya 9:6, NW) Hivyo yeye anaweza kugeuza ule mchafuko wa lugha ulioanza katika Mnara wa Babeli. (Mwanzo 11:6-9) Ni ipi itakayokuwa lugha ya ujumla ya watoto wote wa kidunia wa “Baba ya Milele”? Je! itakuwa ile lugha ya kwanza ya Adamu wa kwanza, ile lugha ambayo Yehova alimpa? Inaelekea kuwa hivyo. Hata iweje, vizuizi vyote vya lugha vitaondolewa kabisa. Utaweza kusafiri mahali po pote na kupashana habari na watu. Utaweza kuwaelewa wao, nao wataweza kukuelewa wewe. Kutakuwako lugha moja kwa wanadamu wote, na ingefaa Biblia nzima ipatikane kwa lugha hiyo. (Linganisha Sefania 3:9.) Katika hiyo lugha dunia yote itajawa na maarifa ya kumjua Yehova “kama vile maji yanavyoifunika bahari.”—Isaya 11:9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki