Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Baba Mwenye Wana Waasi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Wanyama Wasio na Akili Ni Afadhali

      5. Kinyume cha Israeli, ng’ombe na punda huonyeshaje hali fulani ya uaminifu?

      5 Kupitia Isaya, Yehova asema: “Ng’ombe amjua bwana wake, na punda ajua kibanda cha bwana wake; bali Israeli hajui, watu wangu hawafikiri.” (Isaya 1:3)a Watu wanaoishi Mashariki ya Kati wanawafahamu ng’ombe na punda, wanyama wavutao mizigo. Kwa hakika, Wayudea hawangeweza kukanusha kwamba hata wanyama hao wa hali ya chini huonyesha hali fulani ya uaminifu, ufahamu wenye kina kwamba wao ni mali ya bwana-mkubwa fulani. Kuhusu hilo, fikiria aliloshuhudia mtafiti fulani wa Biblia jioni moja katika jiji moja huko Mashariki ya Kati: “Mara kundi lilipoingia ndani ya kuta, likaanza kutawanyika. Kila fahali alimjua mwenyewe kikamilifu na njia ya kwenda nyumbani kwake, wala hakutatanishwa hata kidogo na vijia vingi vilivyopindika-pindika. Punda naye alienda moja kwa moja hadi mlangoni, na kuingia katika ‘hori ya bwana-mkubwa wake.’”

      6. Watu wa Yuda wameshindwaje kutenda kwa kufikiri?

      6 Kwa kuwa mandhari kama hizo zajulikana katika siku ya Isaya, lengo la ujumbe wa Yehova ni wazi: Iwapo hata mnyama asiye na akili hutambua bwana-mkubwa wake na hori yake, mbona watu wa Yuda wamwache Yehova? Kwa kweli “hawafikiri.” Ni kana kwamba hawafahamu kwamba ufanisi wao na hasa uhai wao humtegemea Yehova. Kwa kweli Yehova anawaonyesha rehema yake kwa kuendelea kuwaita Wayudea “watu wangu”!

      7. Twaweza kuonyesha uthamini wetu kwa maandalizi ya Yehova katika njia zipi?

      7 Hatungependa kamwe kutenda bila ufahamu kwa kukosa kuthamini yote ambayo Yehova ametufanyia! Badala yake, twapaswa kumwiga mtunga-zaburi Daudi, aliyesema: “Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote; nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.” (Zaburi 9:1) Kuendelea kutwaa ujuzi juu ya Yehova kutatutia moyo kwa habari hii, kwa maana Biblia yataarifu kwamba “kumjua Mtakatifu ni ufahamu.” (Mithali 9:10) Kutafakari kila siku juu ya baraka za Yehova kutatusaidia kuwa wenye shukrani wala si kumpuuza Baba yetu wa mbinguni. (Wakolosai 3:15) “Atoaye dhabihu za kushukuru, ndiye anayenitukuza,” asema Yehova, “naye autengenezaye mwenendo wake, nitamwonyesha wokovu wa Mungu.”—Zaburi 50:23.

  • Baba Mwenye Wana Waasi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • a Katika muktadha huu, “Israeli” hurejezea ufalme wa Yuda wa makabila mawili.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki