-
Shauri la Yehova Dhidi ya MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
35, 36. Kwa utimizo wa Isaya 19:23-25, ni uhusiano gani uliokuja kuwapo kati ya Misri, Ashuru, na Israeli katika nyakati za kale?
35 Kisha nabii huyo aona kimbele tukio la ajabu: “Katika siku hiyo itakuwako njia kuu itokayo Misri na kufika hata Ashuru; Mwashuri atafika Misri, na Mmisri atafika Ashuru, na Wamisri wataabudu pamoja na Waashuri. Katika siku hiyo Israeli atakuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru, watakuwa baraka kati ya dunia; kwa kuwa BWANA wa majeshi amewabariki, akisema, Wabarikiwe watu wangu Misri; na wewe Ashuru, kazi ya mikono yangu; na wewe Israeli, urithi wangu.” (Isaya 19:23-25) Naam, siku moja, kutakuwepo uhusiano wa kirafiki kati ya Misri na Ashuru. Jinsi gani?
-
-
Shauri la Yehova Dhidi ya MataifaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
37. Mamilioni leo waishije kana kwamba kuna njia kuu kati ya “Ashuru” na “Misri”?
37 Leo, mabaki ya Waisraeli watiwa-mafuta ni “baraka kati ya dunia.” Wao huendeleza ibada ya kweli nao wanawatangazia watu katika mataifa yote ujumbe wa Ufalme. Baadhi ya mataifa hayo ni kama Ashuru, yana uwezo mkubwa wa kijeshi. Mataifa mengine ni yenye uhuru zaidi, labda kama Misri—ambayo wakati mmoja ilikuwa “mfalme wa kusini” katika unabii wa Danieli. (Danieli 11:5, 8) Mamilioni ya watu mmoja-mmoja kutoka katika mataifa yenye uwezo mkubwa wa kijeshi na yale yenye uhuru zaidi wameikubali njia ya ibada ya kweli. Kwa hiyo, watu kutoka katika mataifa yote wameungana katika ‘ibada.’ Hakuna migawanyiko yoyote ya kitaifa miongoni mwao. Wao hupendana, na yaweza kusemwa kikweli kwamba ‘Mwashuri afika Misri, na Mmisri afika Ashuru.’ Ni kana kwamba kuna njia kuu kutoka kwa mmoja hadi kwa mwingine.—1 Petro 2:17.
38. (a) Israeli ‘atakuwaje wa tatu pamoja na Misri na Ashuru’? (b) Kwa nini Yehova asema “Wabarikiwe watu wangu”?
38 Hata hivyo, Israeli ‘apataje kuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru’? Mapema katika “wakati wa mwisho,” walio wengi wa wale wanaomtumikia Yehova duniani walikuwa washiriki wa “Israeli wa Mungu.” (Danieli 12:9; Wagalatia 6:16) Tangu miaka ya 1930, umati mkubwa wa “kondoo wengine,” walio na tumaini la kuishi duniani, umetokea. (Yohana 10:16a; Ufunuo 7:9) Huku wakitoka katika mataifa—yaliyowakilishwa na Misri na Ashuru—wamiminika kwenye nyumba ya ibada ya Yehova na kuwaalika wengine wajiunge nao. (Isaya 2:2-4) Wanafanya kazi ileile ya kuhubiri kama ndugu zao watiwa-mafuta, huvumilia majaribu yaleyale, hudhihirisha uaminifu na uaminifu-maadili uleule, nao hujilisha kwenye meza ileile ya kiroho. Kwa kweli, watiwa-mafuta na “kondoo wengine” ni “kundi moja, mchungaji mmoja.” (Yohana 10:16b) Je, yeyote aweza kutilia shaka kuwa Yehova, aonapo bidii na uvumilivu wao, apendezwa na utendaji wao? Basi haishangazi kwamba yeye atangaza baraka kwao, akisema: “Wabarikiwe watu wangu”!
-