Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Shauri la Yehova Dhidi ya Mataifa
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 35, 36. Kwa utimizo wa Isaya 19:23-25, ni uhusiano gani uliokuja kuwapo kati ya Misri, Ashuru, na Israeli katika nyakati za kale?

      35 Kisha nabii huyo aona kimbele tukio la ajabu: “Katika siku hiyo itakuwako njia kuu itokayo Misri na kufika hata Ashuru; Mwashuri atafika Misri, na Mmisri atafika Ashuru, na Wamisri wataabudu pamoja na Waashuri. Katika siku hiyo Israeli atakuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru, watakuwa baraka kati ya dunia; kwa kuwa BWANA wa majeshi amewabariki, akisema, Wabarikiwe watu wangu Misri; na wewe Ashuru, kazi ya mikono yangu; na wewe Israeli, urithi wangu.” (Isaya 19:23-25) Naam, siku moja, kutakuwepo uhusiano wa kirafiki kati ya Misri na Ashuru. Jinsi gani?

  • Shauri la Yehova Dhidi ya Mataifa
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 38. (a) Israeli ‘atakuwaje wa tatu pamoja na Misri na Ashuru’? (b) Kwa nini Yehova asema “Wabarikiwe watu wangu”?

      38 Hata hivyo, Israeli ‘apataje kuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru’? Mapema katika “wakati wa mwisho,” walio wengi wa wale wanaomtumikia Yehova duniani walikuwa washiriki wa “Israeli wa Mungu.” (Danieli 12:9; Wagalatia 6:16) Tangu miaka ya 1930, umati mkubwa wa “kondoo wengine,” walio na tumaini la kuishi duniani, umetokea. (Yohana 10:16a; Ufunuo 7:9) Huku wakitoka katika mataifa—yaliyowakilishwa na Misri na Ashuru—wamiminika kwenye nyumba ya ibada ya Yehova na kuwaalika wengine wajiunge nao. (Isaya 2:2-4) Wanafanya kazi ileile ya kuhubiri kama ndugu zao watiwa-mafuta, huvumilia majaribu yaleyale, hudhihirisha uaminifu na uaminifu-maadili uleule, nao hujilisha kwenye meza ileile ya kiroho. Kwa kweli, watiwa-mafuta na “kondoo wengine” ni “kundi moja, mchungaji mmoja.” (Yohana 10:16b) Je, yeyote aweza kutilia shaka kuwa Yehova, aonapo bidii na uvumilivu wao, apendezwa na utendaji wao? Basi haishangazi kwamba yeye atangaza baraka kwao, akisema: “Wabarikiwe watu wangu”!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki