-
Yehova Aharibu Kiburi cha TiroUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
16, 17. Ni nini kitakachowapata wakazi wa Tiro jiji hilo liangukapo? (Ona kielezi-chini.)
16 Isaya aendelea na hukumu ya Yehova juu ya Tiro: “Pita katika nchi yako, kama [Mto] Nile, Ee binti wa Tarshishi, hapana tena mshipi wa kukuzuia. Amenyosha mkono wake juu ya bahari, amezitikisa falme; Bwana ametoa amri katika habari za Kanaani, kuziangamiza ngome zake. Naye akasema, Usizidi kufurahi, ewe bikira uliyeaibishwa, binti wa Sidoni, haya, ondoka, uende hata Kitimu; huko nako hutapata raha.”—Isaya 23:10-12.
-
-
Yehova Aharibu Kiburi cha TiroUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
18. Kwa nini Tiro laitwa “bikira . . . binti wa Sidoni,” na hali yake itabadilikaje?
18 Isaya pia asema juu ya Tiro kuwa “bikira . . . binti wa Sidoni,” kuonyesha kwamba washindi wa kigeni hawajaliteka na kulipora jiji hilo hapo awali nalo bado lafurahia hali ya kutoshindwa. (Linganisha 2 Wafalme 19:21; Isaya 47:1; Yeremia 46:11.) Lakini sasa litaharibiwa, na baadhi ya wakazi wake, sawa na wakimbizi, watavuka hadi Kitimu, koloni la Foinike. Hata hivyo, kwa kuwa wamepoteza nguvu zao za kiuchumi, hawatapata raha huko.
-