Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Aharibu Kiburi cha Tiro
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 16, 17. Ni nini kitakachowapata wakazi wa Tiro jiji hilo liangukapo? (Ona kielezi-chini.)

      16 Isaya aendelea na hukumu ya Yehova juu ya Tiro: “Pita katika nchi yako, kama [Mto] Nile, Ee binti wa Tarshishi, hapana tena mshipi wa kukuzuia. Amenyosha mkono wake juu ya bahari, amezitikisa falme; Bwana ametoa amri katika habari za Kanaani, kuziangamiza ngome zake. Naye akasema, Usizidi kufurahi, ewe bikira uliyeaibishwa, binti wa Sidoni, haya, ondoka, uende hata Kitimu; huko nako hutapata raha.”—Isaya 23:10-12.

  • Yehova Aharibu Kiburi cha Tiro
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 18. Kwa nini Tiro laitwa “bikira . . . binti wa Sidoni,” na hali yake itabadilikaje?

      18 Isaya pia asema juu ya Tiro kuwa “bikira . . . binti wa Sidoni,” kuonyesha kwamba washindi wa kigeni hawajaliteka na kulipora jiji hilo hapo awali nalo bado lafurahia hali ya kutoshindwa. (Linganisha 2 Wafalme 19:21; Isaya 47:1; Yeremia 46:11.) Lakini sasa litaharibiwa, na baadhi ya wakazi wake, sawa na wakimbizi, watavuka hadi Kitimu, koloni la Foinike. Hata hivyo, kwa kuwa wamepoteza nguvu zao za kiuchumi, hawatapata raha huko.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki