Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ni Mfalme
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 6. Kwa nini Yehova aiondoa baraka yake nchini humo?

      6 Ili yeyote asikose kuelewa, Isaya afafanua kwa ukamili msiba huo unaokuja naye aeleza sababu yake: “Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika. Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana wameziasi sheria, wameibadili amri, wamelivunja agano la milele. Ndiyo sababu laana imeila dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na hatia, ndiyo sababu watu wanaoikaa dunia wameteketea, watu waliosalia wakawa wachache tu.” (Isaya 24:4-6) Waisraeli walipopewa nchi ya Kanaani, ilikuwa “nchi imiminikayo maziwa na asali.” (Kumbukumbu la Torati 27:3) Licha ya hayo, waliendelea kuitegemea baraka ya Yehova. Iwapo wangeshika amri na maagizo yake kwa uaminifu, nchi ‘ingezaa mazao yake,’ lakini iwapo wangeziasi sheria na amri zake, jitihada zao za kulima nchi ‘zingetumiwa bure’ na nchi ‘haingezaa mazao yake.’ (Mambo ya Walawi 26:3-5, 14, 15, 20) Laana ya Yehova ‘ingeila nchi hiyo.’ (Kumbukumbu la Torati 28:15-20, 38-42, 62, 63) Basi Yuda lazima itarajie kupatwa na laana hiyo.

  • Yehova Ni Mfalme
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 8. (a) Watu ‘wameziasije sheria’ na ‘kuibadili amri’? (b) “Wakuu” wanakuwa wa kwanza ‘kudhoofika’ kwa njia zipi?

      8 Lakini watu “wamelivunja agano la milele.” Wameziasi sheria za Mungu, wakizipuuza. “Wameibadili amri,” wakifuata mazoea ya sheria tofauti na zile ambazo Yehova alitoa. (Kutoka 22:25; Ezekieli 22:12) Basi, watu hao wataondolewa nchini humo. Hukumu inayokuja haitakuwa na rehema yoyote. ‘Watakaodhoofika’ kwanza baada ya Yehova kuondoa ulinzi na upendeleo wake ni “wakuu,” watu mashuhuri. Kwa utimizo wa hayo, uharibifu wa Yerusalemu ukaribiapo, kwanza Wamisri wawafanya wafalme wa Yuda kuwa vibaraka wao, kisha Wababiloni nao wafanya vivyo hivyo. Baadaye, Mfalme Yekonia na washiriki wengineo wa familia ya kifalme ni miongoni mwa watu wa kwanza kupelekwa utekwani Babiloni.—2 Mambo ya Nyakati 36:4, 9, 10.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki