-
Yehova—Uthabiti WetuMnara wa Mlinzi—1988 | Januari 15
-
-
6, 7. (a) Kwa kupatana na Isaya 25:1, inapasa waabudu wa Yehova wamtukuze Yehova kwa ajili ya nini? (b) Ni jinsi gani Isaya 25:2, 3 husimulia jiji fulani? (c) Inaelekea kwamba nabii huyo anaelekeza kwenye jiji gani, na kwa sababu gani?
6 Acheni sisi sasa tugeukie Isaya sura 25. Katika mstari 1, NW sisi tunasoma: “O Yehova, wewe ndiwe Mungu wangu. Mimi nakukweza wewe, mimi naimbilia jina lako, kwa maana wewe umefanya mambo ya ajabu, mashauri kutoka nyakati za mapema, katika uaminifu, katika ustahili wa kuitibariwa.” Waabudu wa Yehova wenye kuitibari wanamtukuza yeye kwa kazi za ajabu ambazo yeye amefanya katikati yao. Lakini Isaya ndipo anapoweka utofautiano wa wazi sana, akisema kwa Yehova: “Kwa maana wewe umefanya jiji liwe rundo la mawe, mji wenye ngome uwe gofu lenye kumomonyoka, mnara-kao wa watu wasiojulikana uwe si jiji, ambalo halitajengwa hata kufika wakati usio dhahiri. . . . Ule mji wa yale mataifa yenye utawala wa ukatili, wao wataogopa [Yehova].”—Isaya 25:2, 3, NW.
-
-
Yehova—Uthabiti WetuMnara wa Mlinzi—1988 | Januari 15
-
-
10. (a) Kwa kupatana na Isaya 25:3, ni jinsi gani ‘ule mji wa mataifa yenye kutawala kwa ukatili’ umelazimishwa kutukuza Yehova, na pia kumwogopa yeye (b) Kwenye Isaya 25:4, 5, ni jinsi gani Isaya anavyosema juu ya Yehova, kuhusu “yule mmoja aliye dhalili na “wale wenye kutawala wenye ukatili”?
10 Katika ule mwaka 1919 Yehova alifungua watu wake wa kweli kutoka mwelekezo-mwelekezo wa “Babuloni yule Mkuu.” Huo ‘mji wa mataifa yenye utawala wa ukatili’ ulilazimashwa umtukuze Yehova katika maana ya kwamba huo ulitakwa uyaone kwa uchungu mwingi yale “mambo ya ajabu” ambayo yeye alitimiza katika kurudisha waabudu wake kwenye utendaji wenye kujaa msukumo mwingi. Wanadini wa bandia wanalazimika kuogopa Yehova, pia, kwa kutazamia mambo ambayo yamo akibani kwa ajili yao. Kwa karne nyingi, viongozi wa kidini wenye kuongoza watu kwa ukatili wamejikweza wenyewe juu ya watu wa kawaida. Lakini sasa Isaya anaongea juu ya Yehova akisema hivi: “Wewe umekuwa boma-imara kwa yule mmoja aliye dhalili, boma-imara kwa yule mmoja maskini katika ile taabu ambayo yeye anayo, kimbilio kutoka ile dhoruba-mvua, uvuli kutoka ile hari, wakati lile pulizo la wenye utawala wa ukatili ni kama dhoruba-mvua dhidi ya ukuta. Kama ile hari katika nchi isiyo na maji, ile kelele ya watu wasiojulikana wewe unatiisha, ile hari unatiisha kwa uvuli wa wingu. Ule mdundo-mtamu wenyewe wa kimuziki ulio wa wenye kutawala kwa ukatili unakuwa uliogandamizwa.”—Isaya 25:4, 5, NW.
-