-
Adui wa Mwisho, Kifo, AangamizwaMnara wa Mlinzi—2014 | Septemba 15
-
-
10. (a) Taja baadhi ya maandiko yanayoonyesha kwamba Yehova ataangamiza kifo tulichorithi kutoka kwa Adamu. (b) Maandiko hayo yanafunua nini kumhusu Yehova na Mwana wake?
10 Naam, Yehova angeweza kumwokoa Paulo. Baada tu ya kutaja “kifuniko,” Isaya aliandika hivi: “Atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote.” (Isa. 25:8) Kama baba anayeondoa hali inayofanya watoto wake wateseke na kufuta machozi yao, Yehova anatazamia kwa shangwe nyingi kuangamiza kifo tulichorithi kutoka kwa Adamu! Yesu anashirikiana naye kutimiza hilo. Andiko la 1 Wakorintho 15:22 linasema hivi: “Kwa maana kama vile katika Adamu wote wanakufa, vivyo hivyo pia katika Kristo wote watafanywa kuwa hai.” Vivyo hivyo, baada ya Paulo kuuliza “Ni nani atakayeniokoa?” alisema hivi: “Shukrani kwa Mungu kupitia Yesu Kristo Bwana wetu!” (Rom. 7:25) Ni wazi kwamba upendo uliomchochea Yehova kuwaumba wanadamu haukupoa baada ya Adamu na Hawa kuasi. Na yule aliyeshirikiana na Yehova kuwafanya wenzi wawili wa kwanza hakupoteza upendo wake wa pekee kuelekea wazao wao. (Met. 8:30, 31) Lakini wanadamu wangeokolewaje?
-
-
Adui wa Mwisho, Kifo, AangamizwaMnara wa Mlinzi—2014 | Septemba 15
-
-
15, 16. (a) Kwa nini ‘adui wa mwisho ni kifo,’ na kitaangamizwa wakati gani? (b) Kulingana na 1 Wakorintho 15:28, Yesu atafanya nini hatimaye?
15 Kufikia mwishoni mwa miaka elfu moja ya utawala wa Ufalme, wanadamu watiifu watakuwa wamewekwa huru kutokana na maadui wote walioletwa na uasi wa Adamu. Biblia inasema hivi: “Kama vile katika Adamu wote wanakufa, vivyo hivyo pia katika Kristo wote watafanywa kuwa hai. Lakini kila mmoja katika daraja lake mwenyewe: Kristo aliye matunda ya kwanza, baadaye wale walio wa Kristo [watawala wenzake] wakati wa kuwapo kwake. Halafu, ule mwisho, wakati atakapomkabidhi ufalme Mungu wake ambaye pia ni Baba yake, wakati atakapokuwa ameangamiza serikali yote na mamlaka yote na nguvu zote. Kwa maana ni lazima atawale akiwa mfalme mpaka Mungu awe ameweka adui zote chini ya miguu yake. Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.” (1 Kor. 15:22-26) Naam, kifo tulichorithi kutoka kwa Adamu kitaangamizwa hatimaye. “Kifuniko” kinachoifunika familia yote ya wanadamu kitakuwa kimeondolewa milele.—Isa. 25:7, 8.
-