-
Itibari Katika Yah Yehova!Mnara wa Mlinzi—1988 | Januari 15
-
-
1, 2. Ni wimbo gani wenye mchachawo wa sifa unaotokezwa kwenye Isaya 26:1-6, na kwa sababu gani?
KULE kushushwa kwa ule ‘mji wa mataifa yenye kutawala kwa ukatili’ kunaitisha wimbo wa ushindi! (Isaya 25:3, NW) Basi, kwa kufaa, unabii kwenye Isaya sura 26, mistari 1 mpaka 6, NW, unatokeza wimbo wenye mchachawo wa kusifu yule Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. Hata sasa huo unaendelea kuimbwa “katika lile bara la Yuda,” neno Yuda likimaanisha “mwenye kuimbiliwa.” Hapa, tena, ile Biblia ya Union Version inatumia ule usemi “Bwana YEHOVA” mahali ambapo jina la kimungu linatajwa mara mbili. Lakini ni yenye kusisimua kama nini yale maneno ya wimbo huo kama yanavyoonekana katika New World Translation, mahali ambapo mtukio huo na mitukio mingine yote ya jina la kimungu inafasiriwa kwa usahihi!
2 Sikiliza sasa wimbo huo wenye mdundo-mtamu wa kimuziki: “Sisi tuna jiji imara. Yeye [Yehova] anaweka wokovu wenyewe kwa ajili ya kuta na boma. Fungueni yale malango, enyi wanaume, kwamba lile taifa lenye uadilifu ambalo linaendeleza mwenendo wa uaminifu lipate kuingia. Ule mwinamio ambao unaungwa mkono sana wewe utaulinda salama katika amani ya kuendelea, kwa sababu ni katika wewe kwamba mmoja anafanywa aitibari. Itibarini katika Yehova, ninyi watu, kwa nyakati zote, kwa maana katika Yah Yehova umo ule Mwamba wa nyakati zisizo dhahiri. Kwa maana yeye amelaza kwenye udhalili wale wanaokikaa kile kimo, ule mji ulioinushwa juu. Yeye anashusha huo, yeye anashusha huo kwenye dunia; yeye analeta huo katika mgusano na mavumbi. Wayo wa mguu utakanyagia-kanyagia chini mji huo, zile nyayo za yule mwenye usumbuo, zile hatua za wale walio dhalili.” Ni shangwe kama nini kuwa miongoni mwa wale wanaotibari ambao sasa wanashiriki katika kuimba wimbo huu—Mashahidi wa Yehova!
-
-
Itibari Katika Yah Yehova!Mnara wa Mlinzi—1988 | Januari 15
-
-
4, 5. (a) Ni nini “ule mji ulioinushwa juu,” na ni jinsi gani watu wa Yehova wanaukanyagia-kanyagia chini katika njia ya usemi wa mfano? (b) Ni wakati gani ule unabii wa Isaya 26:10 unapata utimizo wayo mkubwa, na jinsi gani hivyo? (c) Ni utumizi gani mwingine ambao unabii huu unao?
4 Wakati sisi tunaposikizisha lile onyo kwamba Yehova yuko karibu kulaza kwenye udhalili “ule mji ulioinushwa juu” “Babuloni yule Mkuu,” inatia moyo kuona wenye usumbuo na wadhalili wa dunia wakikumbatia zile habari njema za Ufalme. (Ufunuo 18:2, 4, 5, NW) Katika usemi wa mfano, wao pia, wanakanyagia-kanyagia chini huo “mji ulioinushwa juu,” si kwa kushiriki katika ile kazi ya uangamivu, bali kwa kuwa na sehemu katika kutangaza ile siku ya kisasi cha Yehova juu ya huo mfumo wenye ufisadi. (Isaya 61:1, 2) Kwa miongo ya miaka sasa, Mashahidi wa Yehova wameonyesha fadhili hata kwa waovu kwa kufika kwenye makao yao wakiwa na ule ujumbe wa Ufalme wenye kuokoa uhai. Lakini tokeo limekuwa kama vile ilivyotaarifiwa kwenye Isaya 26:10, NW: “Ingawa yule mwovu apaswe kuonyeshwa pendeleo, ni kwamba tu yeye hatajifunza uadilifu. Katika lile bara la usema-kweli yeye atatenda bila haki na hataona ule uadhimu wa Yehova.”
-