-
Kumrudia Mungu wa KweliJitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
-
-
3, 4. (a) Isaya alitabiri nini kuhusu “sehemu ya mwisho ya hizi siku”? (b) Ni maswali gani yanayohitaji jibu?
3 Miaka zaidi ya 700 kabla ya Kristo, Isaya alikuwa ametabiri kwamba watu wa mataifa yote wangekusanyika kwenye ibada ya kweli ya Yehova na hawangejifunza vita tena. Yeye alisema: “Ni lazima itukie katika sehemu ya kumalizia ya siku kwamba mlima wa nyumba ya Yehova utawekwa imara juu ya kilele cha milima . . . na kwao mataifa yote lazima wamiminike. Na vikundi vingi vya watu kwa hakika vitaenda na kusema: ‘Njooni, enyi watu, na twende juu kwenye mlima wa Yehova, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo; na yeye atatuagiza juu ya njia zake, na sisi tutatembea katika vijia vyake.’ Kwa maana toka Sayuni sheria itatoka, na neno la Yehova kutoka Yerusalemu. Na yeye kwa hakika atatoa hukumu miongoni mwa mataifa na kunyoosha mambo juu ya jamii za watu nyingi. Nao watalazimika kufua panga zao kuwa majembe ya plau na mikuki yao kuwa mikasi ya kupogolea. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.”a—Isaya 2:2-4, NW.
4 Ni ipi kati ya dini zote katika ulimwengu ambayo imekuwa yenye kutokeza katika kutimiza matakwa hayo? Ni nani wamekataa kujifunza vita ijapokuwa magereza, kambi za mateso, na hukumu za kifo?
Upendo wa Kikristo na Kutokuwamo
5. Ni kumbukumbu gani ya kutokuwamo kwa Kikristo ambayo Mashahidi wa Yehova wameimarisha wakiwa watu mmoja mmoja, na kwa nini?
5 Mashahidi wa Yehova wajulikana ulimwenguni pote kwa ajili ya msimamo wao wa kutokuwamo kwa Kikristo wa mtu binafsi kulingana na dhamiri. Wao wamevumilia magereza, kambi za mateso, kuteswateswa, kuhamishwa, na kunyanyaswa katika karne yote ya 20 kwa sababu wamekataa kudhabihu upendo na umoja wao wakiwa kundi la ulimwengu wote la Wakristo waliovutwa kwa Mungu. Katika Ujerumani ya Nazi wakati wa miaka 1933-45, karibu Mashahidi elfu walikufa na maelfu wakafungwa gerezani, kwa sababu ya kukataa kwao kushirikiana na jitihada ya vita ya Hitler. Vivyo hivyo, chini ya Franco katika Hispania iliyokuwa ya Kifashisti hapo kwanza, mamia ya Mashahidi wachanga walienda gerezani na wengi walitumia wastani wa miaka kumi kila mmoja katika magereza ya kijeshi kuliko kujifunza vita. Mpaka wa leo katika nchi kadhaa, Mashahidi wachanga wengi wa Yehova wananyong’onyea katika magereza kwa sababu ya msimamo wao juu ya kutokuwamo kwa Kikristo. Hata hivyo, Mashahidi wa Yehova hawaingilii shughuli za kijeshi za serikali. Kutokuwamo kwa Kikristo kwa Mashahidi kusiko na kigeu-geu katika mambo ya kisiasa kumekuwa mojawapo mambo yasiyobadilika ya imani zao katika mapambano na vita vyote vya karne ya 20. Huwatia alama ya kuwa wafuasi wa kweli wa Kristo na kwawatenganisha na dini za Jumuiya ya Wakristo.—Yohana 17:16; 2 Wakorintho 10:3-5.
6, 7. Mashahidi wa Yehova wamekuja kuelewa nini kuhusu Ukristo?
6 Kwa kushikilia Biblia na kielelezo cha Kristo, Mashahidi wa Yehova huonyesha wanazoea ibada ya Mungu wa kweli, Yehova. Wao watambua upendo wa Mungu kama unavyoonyeshwa katika uhai na dhabihu ya Yesu. Wao waelewa kwamba upendo wa kweli wa Kikristo hutokeza udugu wa ulimwenguni pote usiogawanyika—juu ya migawanyiko ya kisiasa, ya kirangi na kitaifa. Maana yake, Ukristo ni zaidi ya kuwa wa kimataifa; si wa kitaifa, unavuka mipaka ya mataifa, mamlaka, au mapendezi. Huiona jamii ya kibinadamu kuwa familia moja yenye baba mmoja na Muumba mmoja, Yehova Mungu.—Matendo 17:24-28; Wakolosai 3:9-11.
-
-
Kumrudia Mungu wa KweliJitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
-
-
a Sentensi hizo mbili za mwisho zapatikana kwenye “Ukuta wa Isaya” mbele ya majengo ya UM na pia kwenye sanamu moja katika bustani za UM, na kama ilivyo, utimizo wayo ndio moja la malengo ya UM.
-
-
Kumrudia Mungu wa KweliJitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 346]
sanamu ya amani ya um hutoa taarifa hii: “sisi tutafua panga zetu kuwa majembe ya plau”; “Ukuta wa Isaya” hutoa andiko hilo la Kibiblia
-