-
Endelea Kumngojea YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
13. Viongozi wa Yuda watumaini nini, na je, tumaini hilo lastahili?
13 Kisha Isaya afafanua: “Bali ninyi mlisema, La! maana tutakimbia juu ya farasi; basi, ni kweli, mtakimbia; tena, Sisi tutakimbia juu ya wanyama waendao upesi; basi, wale watakaowafuatia watakuwa wepesi.” (Isaya 30:16) Wayudea wanadhani kwamba farasi wenye mbio, badala ya Yehova, ndio watakaowaokoa. (Kumbukumbu la Torati 17:16; Mithali 21:31) Hata hivyo, nabii ajibu kwamba tumaini lao litakuwa ndoto kwa sababu adui zao watawapita. Hata wingi hautawafaidi kitu. “Elfu moja watakimbia kwa kukemewa na mtu mmoja; kwa kukemewa na watano mtakimbia.” (Isaya 30:17a) Majeshi ya Yuda yatajawa na hofu na kukimbia kwa kukemewa na adui wachache tu.a Mwishowe, ni mabaki tu watakaoachwa, wakiwa peke yao, “kama mlingoti juu ya kilele cha mlima, na kama bendera juu ya kilima.” (Isaya 30:17b) Kupatana na unabii huo, jiji la Yerusalemu linapoharibiwa mwaka wa 607 K.W.K., ni mabaki tu wanaosalia.—Yeremia 25:8-11.
-
-
Endelea Kumngojea YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
a Ona kwamba iwapo Yuda ingalikuwa yenye uaminifu, jambo lililo kinyume cha hilo lingalitendeka.—Mambo ya Walawi 26:7, 8.
-