-
Endelea Kumngojea YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
17, 18. Hata katika nyakati za magumu, Yehova huandaaje mwongozo?
17 Isaya aendeleapo kutoa hotuba yake, awakumbusha wanaomsikiliza kwamba shida itakuja. Watu watapata “chakula cha shida na maji ya msiba.” (Isaya 30:20a) Shida na msiba watakazopata wakiwa chini ya mazingiwa zitakuwa za kawaida kama vile chakula na maji zilivyo vitu vya kawaida. Ijapokuwa hivyo, Yehova yuko tayari kuwaokoa wenye mioyo minyofu. “Waalimu [“Mfunzi Mtukufu,” “NW”] wako hawatafichwa tena, ila macho yako yatawaona waalimu wako; na masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.”—Isaya 30:20b, 21.b
18 Yehova ndiye “Mfunzi Mtukufu.” Hakuna mwalimu mwingine anayelingana naye. Ingawa hivyo, watu wawezaje ‘kumwona’ na ‘kumsikia’? Yehova hujifunua kupitia manabii wake, ambao maneno yao yamerekodiwa katika Biblia. (Amosi 3:6, 7) Leo, waabudu waaminifu wasomapo Biblia, ni kana kwamba sauti ya Mungu iliyo kama ya baba inawaelekeza njia ya kufuata na kuwasihi warekebishe mwendo wa tabia yao ili waitembee. Kila Mkristo apaswa kusikiliza kwa makini Yehova asemapo kupitia Biblia na kupitia vichapo vinavyotegemea Biblia, vinavyoandaliwa na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mathayo 24:45-47) Kila mmoja na ajitahidi kuisoma Biblia, kwa ‘maana ni maisha yake.’—Kumbukumbu la Torati 32:46, 47; Isaya 48:17.
-
-
Endelea Kumngojea YehovaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
b Hapo ndipo mahali pekee katika Biblia ambapo Yehova aitwa “Mfunzi Mtukufu.”
-