Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Uwaambie Neno Hili”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • ‘YEHOVA ALINIGUSA KINYWA’

      3. Yehova alifanya jambo gani lisilo la kawaida mwanzoni mwa utume wa Yeremia, naye Yeremia alihisi namna gani?

      3 Kumbuka kwamba mwanzoni wa huduma yake, Yeremia aliambiwa: “Kwa wale wote nitakaokutuma kwao, unapaswa kwenda; na kila jambo nitakalokuamuru, unapaswa kusema. Usiogope kwa sababu ya nyuso zao, kwa maana ‘mimi niko pamoja nawe ili kukukomboa,’ asema Yehova.” (Yer. 1:7, 8) Kisha Mungu akafanya jambo lisilo la kawaida. Yeremia asema: “Yehova akanyoosha mkono wake na kunigusa kinywa changu. Ndipo Yehova akaniambia: ‘Nimeyatia maneno yangu katika kinywa chako. Tazama, nimekupa utume leo.’” (Yer. 1:9, 10) Tangu wakati huo na kuendelea, Yeremia alijua kwamba anazungumza kwa niaba ya Mungu Mweza-Yote.a Kwa msaada wa Mungu, bidii ya Yeremia kwa ajili ya utumishi mtakatifu iliongezeka.—Isa. 6:5-8.

      Picha katika ukurasa wa 34
      Picha katika ukurasa wa 34
      Picha katika ukurasa wa 34

      4. Simulia mifano ya watu wenye bidii ya pekee katika kazi ya kuhubiri.

      4 Leo, Yehova hawagusi kihalisi watumishi wake. Hata hivyo, kupitia roho yake, anawachochea kuwa na tamaa ya kuhubiri habari njema. Wengi wao wana bidii sana. Kwa mfano, fikiria kisa cha Maruja nchini Hispania. Amepooza mikono na miguu kwa zaidi ya miaka 40. Hawezi kuhubiri nyumba kwa nyumba, na kwa hiyo, yeye hutafuta njia nyingine za kuhubiri. Njia moja ni kuandika barua. Maruja humtumia binti yake kuandika. Wakati wa kampeni ya mwezi mmoja, Maruja na binti yake walituma barua zaidi ya 150, kila moja ikiambatana na trakti. Kwa kufanya hivyo, habari njema iliwafikia wengi wa watu katika kijiji jirani. Maruja alimwambia binti yake: “Yoyote kati barua zetu ikimfikia mtu mnyoofu, Yehova atatubariki kwa funzo la Biblia.” Mzee mmoja katika kutaniko lao aandika: “Namshukuru Yehova kwa kutupa akina dada kama Maruja, ambao huwafundisha wengine wathamini mambo yaliyo ya maana.”

  • “Uwaambie Neno Hili”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • a Katika kisa hiki, kama ilivyo katika visa vingine vingi, Yehova aliwakilishwa na malaika aliyezungumza kana kwamba ni Yehova mwenyewe.—Amu. 13:15, 22; Gal. 3:19.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki