Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Cha Biblia Namba 15—Ezra
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 8. Eleza mfululizo wa matukio yaliyoongoza kwenye mwisho wa miaka 70 ya ukiwa.

      8 Baki larejea (1:1–3:6). Roho yake ikiwa imeamshwa na Yehova, Koreshi mfalme wa Uajemi atoa amri kwa Wayahudi warejee na kujenga nyumba ya Yehova katika Yerusalemu. Awasihi Wayahudi wale ambao huenda wakabaki Babuloni wachange kwa ukarimu kuelekea kazi hiyo na apanga kwa Wayahudi wanaorejea wachukue vyombo vya lile hekalu la awali. Mmoja ambaye ni kiongozi kutoka kabila la kifalme la Yuda na mzao wa Mfalme Daudi, Zerubabeli (Sheshbaza), apewa mgawo wa kuwa liwali ili kuongoza waliofunguliwa, na Yeshua (Yoshua) ndiye kuhani mkuu. (Ezra 1:8; 5:2; Zek. 3:1) Baki ambalo huenda hesabu yalo ilikuwa 42,360 la watumishi wa Yehova waaminifu, kutia wanaume, wanawake, na watoto, lafunga safari hiyo ndefu. Kufikia mwezi wa saba, kulingana na kalenda ya Kiyahudi, wamekalia miji yao, na kisha wakusanyika kule Yerusalemu ili kutoa dhabihu kwenye kituo cha madhabahu ya hekalu na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda katika vuli ya 537 K.W.K. Hivyo miaka 70 ya ukiwa yamalizika kwa wakati barabara!b

  • Kitabu Cha Biblia Namba 15—Ezra
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 14. Kitabu cha Ezra chaonyesha nini kuhusu unabii mbalimbali wa Yehova?

      14 Kitabu cha Ezra ni chenye mafaa, kwanza, katika kuonyesha usahihi usio na kosa ambao katika huo unabii mbalimbali wa Yehova hutimizwa. Yeremia, ambaye alikuwa ametabiri kwa usahihi sana ukiwa wa Yerusalemu, pia alitabiri kurejeshwa baada ya miaka 70. (Yer. 29:10) Kwa wakati barabara, Yehova alionyesha fadhili zake za upendo katika kuleta watu wake, baki jaminifu, kurejea tena katika Bara la Ahadi ili kuendeleza ibada ya kweli.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki