Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Tafadhali Turuhusu Turudi Nyumbani”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Aprili 1
    • “Kwa Kuwa Nitamhurumia Kabisa”

      Yehova alikuwa na uhusiano wa pekee na Waisraeli. Alisema hivi: “Mimi nimekuwa Baba kwa Israeli; naye Efraimu, yeye ni mzaliwa wangu wa kwanza.” (Yeremia 31:9) Bila shaka, baba mwenye upendo hawezi kukataa kumkaribisha mwana aliyetubu kikweli. Ona jinsi Yehova anavyowaonyesha watu wake hisia kama za Baba.

      “Je, Efraimu ni mwana mwenye thamani kwangu, au mtoto anayetendewa kwa upendo? Kwa maana kwa kiasi ninachosema vibaya juu yake bila shaka nitamkumbuka zaidi.” (Mstari wa 20) Maneno hayo ni yenye huruma kama nini! Kama mzazi mwenye upendo lakini mwenye msimamo thabiti, Mungu alilazimika kusema “vibaya” kuwahusu watoto wake tena na tena akiwaonya kuhusu njia zao mbaya. Walipokataa kumsikiliza kwa kiburi, aliruhusu wapelekwe utekwani—ni kana kwamba alifanya waondoke nyumbani. Hata ingawa alilazimika kuwaadhibu, hakuwasahau kamwe. Baba mwenye upendo hawasahau watoto wake. Hata hivyo, Yehova alihisije alipoona watoto wake wametubu kikweli?

      “Matumbo yangu yamekuwa na msukosuko kwa ajili yake.b Kwa kuwa nitamhurumia kabisa.” (Mstari wa 20) Yehova alitamani sana watoto wake wamrudie. Toba yao ya kweli iligusa moyo wake, na akatamani sana wamrudie. Kama baba anayetajwa katika mfano wa Yesu wa mwana mpotevu, Yehova ‘aliwasikitikia,’ na akatamani kuwakaribisha watoto wake warudi nyumbani.—Luka 15:20.

      “Yehova Aliniruhusu Nirudi Nyumbani!”

      Maneno yaliyo katika andiko la Yeremia 31:18-20 yanatusaidia kufahamu huruma nyororo na rehema za Yehova. Mungu hawasahau watu ambao wakati fulani walikuwa wakimtumikia. Vipi ikiwa watu hao wanataka kumrudia? Mungu yuko ‘tayari kuwasamehe.’ (Zaburi 86:5) Siku zote, anawakubali wote ambao wanakuja kwake wakiwa wametubu kikweli. (Zaburi 51:17) Pia, anafurahia kuwakaribisha nyumbani.—Luka 15:22-24.

  • “Tafadhali Turuhusu Turudi Nyumbani”
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Aprili 1
    • b Kitabu fulani cha mwongozo wa watafsiri wa Biblia kinaeleza hivi kuhusu hali hiyo ya mfano ya msukosuko wa matumbo: “Wayahudi waliona kwamba sehemu za ndani za mwili zilikuwa kiini cha hisia.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki