Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unaweza Kufaidika Kutokana na Agano Jipya
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • 5. Kwa nini Yehova alitabiri kuhusu agano jipya?

      5 Hivyo basi, tunaweza kuona ni kwa nini hata wakati ambapo agano la Sheria lilikuwa likitumika, Mungu alimwagiza Yeremia atabiri kuhusu agano lingine, agano jipya. Kwa sababu ya upendo na fadhili zake, Yehova alitaka kutoa msaada wa kudumu kwa ajili ya watu wa mataifa yote. Kupitia Yeremia, Mungu alisema hivi kuhusu wale ambao wangehusishwa katika agano ambalo lingefanywa baadaye: “Nitalisamehe kosa lao, na dhambi yao sitaikumbuka tena.” (Yer. 31:34) Ingawa ahadi hiyo ilitolewa katika siku za Yeremia, inatoa tumaini zuri kwa wanadamu wote. Jinsi gani?

      6, 7. (a) Wengine huhisi namna gani kuhusiana na hali yao yenye dhambi? (b) Kwa nini kuchunguza agano jipya kunaweza kukutia moyo?

      6 Sisi si wakamilifu, na mara kwa mara tunajikuta katika hali zinazotukumbusha hilo. Kwa mfano, ndugu mmoja alikuwa akijitahidi kushinda zoea fulani baya. Anasema: “Nilipojikuta nimerudia zoea hilo, niliumia sana moyoni. Nilifikiri hakuna lolote ninaloweza kufanya ili kupata msamaha. Nilishindwa kusali. Nilikuwa nikianza kwa kusema, ‘Yehova, sijui kama utaisikiliza sala hii, lakini . . .’” Watu fulani ambao wamerudia zoea fulani au kufanya dhambi wamehisi kana kwamba “wingu kubwa” linazuia sala zao zisimfikie Mungu. (Omb. 3:44) Wengine wamesumbuliwa na kumbukumbu za makosa yao ya wakati uliopita, miaka mingi baadaye. Hata Wakristo wakomavu huenda wakasema mambo ambayo baadaye wanajuta kwamba waliyasema.—Yak. 3:5-10.

      7 Hakuna yeyote kati yetu anayepaswa kufikiri kwamba hawezi kamwe kutumbukia katika mwenendo usiofaa. (1 Kor. 10:12) Hata mtume Paulo alitambua kwamba mara kwa mara alikuwa akikosea. (Soma Waroma 7:21-25.) Kuhusiana na hilo, tunapaswa kukumbuka agano jipya. Mungu aliahidi kwamba jambo moja kuu kuhusu agano jipya ni kwamba hatazikumbuka dhambi tena. Faida isiyo na kifani ya agano jipya! Lazima kutabiri hilo kulimchochea Yeremia sana, nasi pia tunaweza kuchochewa tunapojifunza mengi kuhusu agano jipya na kuona jinsi tunavyopata faida kutokana nalo.

  • Unaweza Kufaidika Kutokana na Agano Jipya
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • 8, 9. Ilimgharimu Yehova nini ili kuandaa msamaha wa dhambi?

      8 Unapopata kumjua Yehova vizuri, unaendelea kutambua jinsi alivyo mwenye fadhili na rehema kuwaelekea wanadamu wasio wakamilifu. (Zab. 103:13, 14) Alipotabiri kuhusu agano jipya, Yeremia alikazia kwamba Yehova ‘angesamehe kosa lao’ na dhambi yao hangeikumbuka tena. (Yer. 31:34) Lazima Yeremia alikuwa na hamu ya kujua jinsi ambavyo Mungu angefanya hivyo. Angalau alielewa kwamba Mungu alipozungumzia agano jipya, alimaanisha kwamba kungekuwa na makubaliano, au mapatano, kati Yake na wanadamu. Kwa njia fulani, kupitia agano hilo, Yehova angetimiza yale ambayo alimwongoza Yeremia kuandika, kutia ndani kuwasamehe wanadamu. Habari zaidi zingepatikana wakati ambapo Mungu angefunua zaidi kusudi lake, kutia ndani yale ambayo Masihi angefanya.

      9 Huenda umeona wazazi wanaowaendekeza watoto wao, kwa kutowatia nidhamu. Je, unafikiri ndivyo alivyo Yehova? Sivyo, hata kidogo! Hilo laonekana wazi kutokana na jinsi agano jipya lilivyotekelezwa. Badala tu ya kufutilia mbali dhambi, kwa uangalifu mwingi sana, Mungu alitilia maanani viwango vyake vya haki kwa kuandaa msingi halali wa kusamehe dhambi, jambo lililomgharimu sana. Unaweza kuelewa jambo hilo kwa kufikiria yale ambayo Paulo aliandika alipokuwa akizungumzia agano jipya. (Soma Waebrania 9:15, 22, 28.) Paulo alitaja “kuachiliwa huru kwa fidia” na kusema kwamba “damu isipomwagwa hakuna msamaha unaotokea.” Katika agano jipya, hilo halikumaanisha damu ya dhabihu za ng’ombe dume au mbuzi kama ilivyokuwa chini ya Sheria. Agano jipya lilianzishwa kupitia damu ya Yesu. Kwa msingi wa dhabihu hiyo kamilifu, Yehova angeweza ‘kusamehe makosa na dhambi’ milele. (Mdo. 2:38; 3:19) Lakini ni nani ambao wangekuwa katika agano hilo jipya na kupata msamaha huo? Si taifa la Kiyahudi. Yesu alisema kwamba Mungu angewakataa Wayahudi, wale waliokuwa wakitoa dhabihu za wanyama chini ya Sheria, Naye angeligeukia taifa lingine. (Mt. 21:43; Mdo. 3:13-15) Taifa hilo likaja kuwa “Israeli wa Mungu,” yaani, Wakristo waliotiwa mafuta kwa roho takatifu. Kimsingi, agano la Sheria lilikuwa kati ya Mungu na Israeli wa asili, lakini agano jipya ni kati ya Yehova Mungu na Israeli wa kiroho, Yesu akiwa Mpatanishi.—Gal. 6:16; Rom. 9:6.

      Picha katika ukurasa wa 172

      10. (a) “Chipukizi” la Daudi ni nani? (b) Wanadamu wanaweza kufaidika jinsi gani kutokana na “chipukizi” hilo?

      10 Yeremia, akizungumzia Yule anayekuja, yaani, Masihi, alimwita “chipukizi” la Daudi. Hilo linafaa. Hata Yeremia alipokuwa nabii, nasaba ya kifalme ya familia ya Daudi ilikuwa imekatishwa. Hata hivyo, kisiki cha mti uliowakilisha nasaba hiyo hakikuwa kimekufa. Baadaye, Yesu alizaliwa katika ukoo wa Mfalme Daudi. Angeweza kuitwa “Yehova Ni Uadilifu Wetu,” jina linalokazia kwamba Mungu anahangaikia sana sifa hiyo. (Soma Yeremia 23:5, 6.) Yehova alimtoa Mwana wake wa pekee ateseke na kufa hapa duniani. Kisha Yehova, kulingana na haki yake, alitumia thamani ya dhabihu ya fidia ya “chipukizi” la Daudi kuwa msingi wa msamaha. (Yer. 33:15) Hilo liliwafungulia njia wanadamu kadhaa kutangazwa kuwa “waadilifu kwa ajili ya uzima” na kutiwa mafuta kwa roho takatifu wawe washiriki wa agano jipya. Uthibitisho mwingine wa kwamba Mungu anapendezwa na uadilifu ni kwamba wengine ambao si sehemu ya agano hilo jipya wanaweza na wanafaidika kutokana na agano hilo, kama tutakavyoona.—Rom. 5:18.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki