-
Kujifunza Kupata Furaha Katika Kumhofu YehovaMnara wa Mlinzi—1995 | Machi 15
-
-
14, 15. (a) Alipokuwa akitabiri juu ya kurudishwa kwa Israeli kutoka katika utumwa wa Babiloni, Yehova aliahidi kuwapa watu wake nini? (b) Yehova alifanya nini ili kutia hali ya kumhofu Mungu mioyoni mwa watu wake? (c) Kwa nini Israeli waligeuka kando kutoka kwa njia za Yehova?
14 Yehova aliahidi kwamba angewapa watu wake moyo huo umhofuo Mungu. Yeye alitabiri kurudishwa kwa Israeli akasema hivi, kama tusomavyo kwenye Yeremia 32:37-39: “Nitawaleta tena hata mahali hapa, nami nitawakalisha salama salimini; nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; nami nitawapa moyo mmoja, na njia moja, wapate kunicha [“kunihofu,” NW] sikuzote; kwa mema yao, na ya watoto wao baada yao.” Katika mstari wa 40, ahadi ya Mungu inakaziwa hivi: “Nami nitatia kicho changu [“kunihofu kwangu,” NW] mioyoni mwao, ili wasiniache.” Katika 537 K.W.K., Yehova kwa hakika aliwarudisha Yerusalemu, kama vile alivyokuwa ameahidi. Lakini namna gani ile sehemu nyingine ya ahadi hiyo—kwamba angewapa ‘moyo mmoja wapate kumhofu sikuzote’? Kwa nini taifa la Israeli la kale lilimwacha Yehova baada ya yeye kuwarudisha kutoka Babiloni, hivi kwamba hekalu lao liliharibiwa katika 70 W.K., lisipate kujengwa tena kamwe?
-
-
Kujifunza Kupata Furaha Katika Kumhofu YehovaMnara wa Mlinzi—1995 | Machi 15
-
-
16. Yehova ametia hofu ya kimungu katika mioyo ya nani?
16 Hata hivyo, ahadi ya Yehova ya kutia hofu ya kimungu mioyoni mwa watu wake haikushindwa. Yeye alifanya agano jipya pamoja na Israeli wa kiroho, wale Wakristo aliowatolea tumaini la kimbingu. (Yeremia 31:33; Wagalatia 6:16) Katika 1919, Mungu aliwarudisha kutoka katika utumwa wa Babiloni Mkubwa, ile milki ya ulimwengu ya dini isiyo ya kweli. Yeye ametia imara hali ya kumhofu mioyoni mwao. Hilo limeleta manufaa nyingi sana kwao na kwa “umati mkubwa,” walio na tumaini la uhai wakiwa raia wa kidunia wa Ufalme. (Yeremia 32:39; Ufunuo 7:9, NW) Hali ya kumhofu Yehova imekuja kuwa mioyoni mwao pia.
-