Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Baruku Mwandishi Mwaminifu wa Yeremia
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Agosti 15
    • Usijitafutie “Makuu”

      Baruku alitaabika alipokuwa akiandika kitabu cha kwanza. Alisema hivi: “Ole wangu, sasa, kwa maana Yehova ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu! Nimechoka kwa sababu ya kuugua kwangu, nami sikupata mahali pa kupumzika.” Kwa nini alitaabika?—Yeremia 45:1-3.

      Hakuna jibu la moja kwa moja linalotolewa. Lakini hebu jaribu kuwazia hali ya Baruku. Haikosi kwamba kuandika kuhusu maonyo yaliyotolewa kwa kipindi cha miaka 23 juu ya taifa la Israeli na Yuda kulimfanya aone waziwazi uasi-imani wao na jinsi Yehova alivyowakataa. Hapana shaka Baruku alishtuka kusikia uamuzi wa Yehova wa kuharibu Yerusalemu na Yuda na kupeleka taifa hilo uhamishoni Babiloni kwa miaka 70. Yehova alifunua habari hizo mwaka huohuo na huenda ikawa ziliandikwa katika kitabu hicho cha kukunjwa. (Yeremia 25:1-11) Isitoshe, angeweza kupoteza cheo chake na kazi yake kwa sababu ya kumuunga mkono Yeremia katika kipindi hicho muhimu.

      Hata ingawa sababu ya kutaabika kwake haijulikani waziwazi, Yehova mwenyewe aliingilia kati ili kumsaidia Baruku atilie maanani hukumu iliyokaribia. Yehova alisema hivi: “Kile ambacho nimekijenga ninakibomoa, na kile ambacho nimekipanda ninaking’oa, ndiyo, nchi yote.” Kisha akamshauri Baruku hivi: “Na wewe unaendelea kujitafutia makuu. Usiendelee kuyatafuta.”—Yeremia 45:4, 5.

      Yehova hakutaja kihususa mambo hayo “makuu.” Lakini haikosi kwamba Baruku alijua mambo hayo, ambayo labda yalitia ndani tamaa ya kibinafsi ya kupata makuu, umashuhuri, au mali. Yehova alimshauri aone mambo kihalisi na kukumbuka mambo ambayo yangetokea: “Ninaleta msiba juu ya wote wenye mwili, . . . nami nitakupa wewe nafsi yako kuwa nyara katika mahali pote utakapoenda.” Uhai wa Baruku ungehifadhiwa popote ambapo angeenda, na hicho ndicho kitu cha thamani zaidi ambacho alikuwa nacho.—Yeremia 45:5.

  • Baruku Mwandishi Mwaminifu wa Yeremia
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Agosti 15
    • Baruku alipokumbushwa kwamba hakuna wakati wa kujitafutia “makuu” katika siku za mwisho za ufalme wa Yuda, inaonekana alitii shauri hilo kwa sababu alipokea nafsi yake kuwa nyara. Inafaa tutii shauri hilo, kwa kuwa sisi pia tunaishi katika siku za mwisho za mfumo wa mambo. Kama Baruku, Yehova anaahidi kutuhifadhi hai. Je, tunaweza kutii vikumbusho hivyo kama Baruku?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki