Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Utatembea Pamoja na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 1
    • 11. Kulingana na Yeremia 6:16, Yehova aliwapa watu wake mfano gani wenye kugusa moyo, lakini wao waliitikiaje?

      11 Je, tunaliruhusu Neno la Mungu lituongoze kwa ukaribu hivyo? Ni muhimu kutua kidogo wakati mwingine na kujichunguza kwa unyoofu. Ona mstari utakaotusaidia kufanya hivyo: “Yehova amesema hivi: ‘Simameni tuli katika njia, na kuona, na kuuliza juu ya barabara za zamani za kale, mahali ambapo sasa pana njia nzuri; na mtembee ndani yake, na kustarehesha nafsi zenu.’” (Yeremia 6:16) Maneno hayo yanaweza kutukumbusha kuhusu msafiri anayesimama kwenye makutano ya barabara ili kuulizia njia. Kwa njia ya kiroho, Waisraeli waliomwasi Yehova walipaswa kufanya vivyo hivyo. Walipaswa kurudi katika “barabara za zamani za kale.” Hiyo “njia nzuri” ndiyo njia ambayo babu zao walitembea ndani yake, na ambayo taifa lao lilikuwa limeiacha kwa upumbavu. Inasikitisha kwamba Waisraeli walikaidi kikumbusho hicho chenye upendo kutoka kwa Yehova. Mstari huohuo unaendelea kusema hivi: “Lakini waliendelea kusema: ‘Hatutatembea.’” Hata hivyo, watu wa Mungu leo wameitikia kwa njia tofauti.

      12, 13. (a) Wafuasi watiwa-mafuta wa Kristo wameitikiaje lile shauri katika Yeremia 6:16? (b) Tunaweza kujichunguzaje kuhusiana na jinsi tunavyotembea leo?

      12 Tangu mwishoni mwa karne ya 19, wafuasi watiwa-mafuta wa Kristo wametii shauri la Yeremia 6:16. Wakiwa kikundi, wamewaongoza wengine warudi kwa moyo wote katika “barabara za zamani za kale.” Tofauti na dini zinazodai kuwa za Kikristo, wao wameshikamana kwa uaminifu na “kielelezo cha maneno yenye afya” kilichowekwa na Yesu Kristo na kufuatwa na wafuasi wake waaminifu wa karne ya kwanza W.K. (2 Timotheo 1:13) Mpaka leo, watiwa-mafuta wanasaidiana na kuwasaidia waandamani wao, “kondoo wengine” kufuata njia ya maisha yenye afya na yenye furaha ambayo imeachwa na dini zinazodai kuwa za Kikristo.—Yohana 10:16.

      13 Kwa kuandaa chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa, jamii ya mtumwa mwaminifu imewasaidia mamilioni ya watu kupata “barabara za zamani za kale” na kutembea pamoja na Mungu. (Mathayo 24:45-47) Je, uko miongoni mwao? Ikiwa ndivyo, unaweza kufanya nini ili usipeperushwe na kufuata njia yako mwenyewe? Ni jambo la hekima kutua kidogo na kuchunguza jinsi unavyotembea maishani. Ikiwa unasoma kwa ukawaida Biblia na vichapo vinavyoifafanua na kuhudhuria programu za mafundisho zinazopangwa na watiwa-mafuta leo, basi unazoezwa kutembea pamoja na Mungu. Na unapotumia kwa unyenyekevu shauri unalopewa, kwa kweli unatembea pamoja na Mungu na kufuata “barabara za zamani za kale.”

  • Je, Utatembea Pamoja na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 1
    • Kuna Baraka Gani?

      17. Tukitembea katika njia ya Yehova, ‘tutastareheshaje’ nafsi zetu?

      17 Tukitembea pamoja na Yehova Mungu tutakuwa na maisha yenye kuridhisha. Kumbuka kile ambacho Yehova aliwaahidi watu wake kuhusu kutafuta “njia nzuri.” Aliwaambia hivi: “Mtembee ndani yake, na kustarehesha nafsi zenu.” (Yeremia 6:16) “Kustarehesha” kunamaanisha nini? Je, kujistarehesha kunamaanisha kuwa na maisha ya raha na anasa? Hapana. Yehova anaandaa kitu bora zaidi, kitu ambacho hata watu ambao ni matajiri zaidi hawapati kwa urahisi. Kustarehesha nafsi yako ni kupata amani ya akili, shangwe, na uradhi wa kiroho. Starehe hiyo inamaanisha kwamba unaweza kuwa na uhakika kwamba umechagua njia bora maishani. Amani hiyo ya akili haipatikani kwa urahisi katika ulimwengu huu wenye shida!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki